Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Eric James Shigongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Primary Question

MHE. ERIC J. SHIGONGO K.n.y. MHE. SALMA R. KIKWETE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga kivuko kutoka Mchinga Moja kwenda Mchinga Mbili ili kurahisisha huduma kwa wananchi ikiwemo wanafunzi wanaovuka bahari kwa miguu kwenda Shule ya Sekondari Mchinga?

Supplementary Question 1

MHE. ERIC J. SHIGONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninashukuru sana. Kwa sababu mahitaji ya wananchi wa Mchinga ni kufanya biashara na kuongeza kipato, na kivuko hiki ni muhimu sana kwa ajili ya maendeleo ya uchumi wa jimbo hili. Ningependa kupata tamko rasmi la Serikali kwamba ni lini hasa watarajie kwamba ahadi hii ya Serikali itatekelezwa? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshi mi wa Mwenyekiti, ahsante sana na naomba kujibu swali dogo la nyongeza Mheshimiwa Shigongo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu katika swali la msingi, Mheshimiwa Mbunge ametaka kujua ni lini hasa. Nimemueleza hapa kwamba tulishafanya tathmini, na daraja hilo linahitaji shilingi milioni 147, na imetengwa katika bajeti ambayo tutapitisha katika Bunge hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo katika mwaka wa fedha unaokuja daraja hili litajengwa, na hiyo nina uhakika kwa asilimia 100. Ahsante sana.

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. ERIC J. SHIGONGO K.n.y. MHE. SALMA R. KIKWETE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga kivuko kutoka Mchinga Moja kwenda Mchinga Mbili ili kurahisisha huduma kwa wananchi ikiwemo wanafunzi wanaovuka bahari kwa miguu kwenda Shule ya Sekondari Mchinga?

Supplementary Question 2

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kwa nafasi ili na mimi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto zilizopo Mchinga zinafanana sana na Changamoto za Wilaya ya Nkasi katika Kata ya Isunta na Kata ya Namanyele ambako kivuko hicho kimekuwa kikiathiri sana wanafunzi wanaokwenda Mkangale primary pamoja na sekondari ya Mkangale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini Serikali itajenga kivuko hiki ili kuwasaidia watoto ambao wamekuwa wakipata shida sana?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba kijibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Aida Khenani, Mbunge wa Nkasi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwamba, kama nilivyoeleza awali, madaraja yote yakiwemo yaliyo katika jimbo lake tumeshayafanyia tathmini, na mengi tunatarajia kuyaweka katika bajeti hii inayokuja ya mwaka 2022/2023. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutatekeleza ahadi hii ambayo Serikali imeahidi. Ahsante sana.