Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 4 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 29 2022-02-04

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. ERIC J. SHIGONGO K.n.y. MHE. SALMA R. KIKWETE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga kivuko kutoka Mchinga Moja kwenda Mchinga Mbili ili kurahisisha huduma kwa wananchi ikiwemo wanafunzi wanaovuka bahari kwa miguu kwenda Shule ya Sekondari Mchinga?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Salma Rashid Kikwete, Mbunge wa Jimbo la Mchinga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua uwepo wa changamoto ya kivuko katika barabara ya Mchinga –Kijiweni, eneo la kutoka Mchinga Moja kwenda Mchinga Mbili lililo katika Jimbo la Mchinga, Wilaya ya Lindi. Serikali kupitia TARURA Mkoa wa Lindi, imeshafanya tathimini ya awali ya kutatua changamoto hiyo ambapo kiasi cha shilingi milioni 147 kitaweza kujenga kivuko cha waenda kwa miguu (pedestrian suspended bridge).

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika bajeti ya mwaka wa fedha 2022/2023 TARURA Wilaya ya Lindi itatenga bajeti ya kiasi cha shilingi milioni 147 kwa ajili ya kujenga kivuko cha waenda kwa miguu. Aidha, ujenzi wa kivuko hicho utaondoa changamoto ya usafiri na usafirishaji katika eneo hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, Serikali itaendelea kuboresha miundombinu ya barabara katika Jimbo la Mchinga kulinga na upatikanaji wa fedha.