Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ali Juma Mohamed

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shaurimoyo

Primary Question

MHE. ALI JUMA MOHAMED aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuwatafutia ajira na fursa mbalimbali nje ya nchi?

Supplementary Question 1

MHE. ALI JUMA MOHAMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri nilikuwa na maswali mawili madogo ya nyongeza.

Je, Serikali ina mpango gani kwa kutumia ofisi zetu za kibalozi kuwasaidia wale vijana wetu wa Kitanzania ambao tayari wameshapata fursa ya kufanyakazi nje ya nchi, lakini mara kwa mara wamekuwa wakipata matatizo na shida ambazo wanakosa kusaidiwa?

Lakini la pili Serikali ina takwimu rasmi za vijana wote ambao wanafanyakazi nje ya nchi?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimshukuru sana Mheshimiwa Mohamed kwa kuangalia sana haya maslahi ya ajira ya Watanzania nimpongeze sana kwa kazi hiyo nzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ofisi yetu, Ofisi ya Waziri Mkuu inashirikiana vizuri na Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje kwa kuhakikisha kwamba masuala haya yanaratibiwa vizuri na hata hivi sasa tumekwisha kuanza utambuzi huo wa vijana wapo ambao walikuwa wanaenda wenyewe bila kutoa taarifa kwenye ubalozi au kwenye nchi na wamekuwa wakipata matatizo mbalimbali tumewaomba na tumetoa rai kwamba waendelee kujisajili kwenye Balozi zetu.

Lakini zaidi ya hapo pia katika mikataba ambayo tumeingia sasa maalum, kwa mfano Qatar tunakuwa na Kombe la Dunia hivi karibuni wafanyakazi wengi tunatarajia kuwapeleka kule na waweze kupata ajira.

Kwa hiyo, haya tunayaratibu vizuri kupitia Wizara ya Mambo ya Nje kwa kushirikiana na balozi zetu huko nchini na hivi karibuni mmeona Balozi wa Ubelgiji alitoa takwimu za maeneo ambayo Watanzania wangeweza kuchangamkia kuweza kupata ajira. Kwa hiyo uratibu upo kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu katika maeneo hayo.