Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 4 Youth, Disabled, Labor and Employment Ofisi ya Waziri Mkuu: Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu 27 2022-02-04

Name

Ali Juma Mohamed

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shaurimoyo

Primary Question

MHE. ALI JUMA MOHAMED aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwatafutia ajira na fursa mbalimbali nje ya nchi?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ali Juma Mohamed, Mbunge wa Shaurimoyo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatekeleza mpango mikakati ifuatayo ili kuunganisha vijana na fursa za ajira nje ya nchi: -

(i) Imeingia makubaliano (bilateral agreements) na baadhi ya nchi zenye fursa za ajira duniani.

(ii) Imeweka mwongozo wa kuratibu shughuli za Wakala Binafsi wa Huduma za Ajira ili kuwezesha shughuli za kuunganisha Watanzania na fursa za ajira nje ya nchi kufanyika kwa kuzingatia haki za msingi za wafanyakazi na viwango vya kazi vinavyokubalika na Shirika la Kazi Duniani (ILO). Hadi sasa jumla ya Wakala 58 wamesajiliwa na kupewa leseni, kati ya hao Wakala watano wanajishughulisha na kuwaungaunisha watafuta ajira nje ya nchi.

(iii) Kujenga mfumo wa kielektroniki wa huduma za ajira utakaorahisisha na kuweka uwazi katika kuratibu upatikanaji wa fursa za ajira nje ya nchi; mchakato wa kuandaa Watanzania wenye sifa pamoja na kufuatilia hali za Watanzania wakiwa wanafanya kazi nje ya nchi. Mfumo unatarajiwa pia kukamilika na kuanza kutumika kabla ya mwezi Juni, 2022.

(iv) Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la tatu katika mpango huo ni kutekeleza Programu ya Taifa ya Mafunzo ya Ujuzi hususani kupitia mafunzo ya uanagezi pamoja na utarajali ili kuwezesha vijana husika kuwa na ujuzi stahiki kufanya kazi nje ya nchi.

(v) Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la tano baadhi ya machache hayo nikiyataja kwa sababu ya muda kufanyia marekebisho Sheria ya Huduma za Ajira ya mwaka 1999 pamoja na Kanuni za mwaka 2014 ili ziweze kuendana na mazingira ya sasa ahsante.