Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Primary Question

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani mahsusi wa kuhakikisha vijana wote wanaoomba mikopo ya Elimu ya Juu wanapata mikopo hiyo kama walivyoomba?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kunipatia nafasi ya swali la nyongeza. Kwa kuwa, idadi ya wanafunzi wanaomaliza darasa la saba, kidato cha nne na kidato cha sita inaongezeka mwaka hadi mwaka; na kwa kuwa, bajeti yetu na uwezo wetu wa kuwagharimia kupata mikopo sio mkubwa sana. Je, Serikali haioni sasa ni muda muafaka kuanza maongezi na mazungumzo na benki za kibiashara, ili Serikali iwadhamini vijana wetu ambao wanakosa mikopo, ili wapate mikopo kupitia benki za biashara kwa riba nafuu ambayo Serikali itaweza kuwadhamini?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, naomba sasa kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Kikoyo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa vile ametuletea pendekezo, ametuletea wazo. Mheshimiwa Mwenyekiti na Waheshimiwa Wabunge naomba nilihakikishie Bunge lako tunaomba tulibebe pendekezo hili la Mheshimiwa Dkt. Kikoyo twende tukakae chini, tulifanyie kazi, tufanye tathmini ya kina na pindi tutakapoona kwamba, jambo hili linafaa, basi tutakuja kulieleza kwenye Bunge lako Tukufu ni namna gani ya kuliendea jambo hili. Ahsante sana.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani mahsusi wa kuhakikisha vijana wote wanaoomba mikopo ya Elimu ya Juu wanapata mikopo hiyo kama walivyoomba?

Supplementary Question 2

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Kiuhalisia Wizara ya Elimu ni miongoni mwa Wizara ambayo inaonekena inatengewa bajeti kubwa, lakini unakuta pesa nyingi katika Wizara hii ni pesa za mikopo ya elimu ya juu ambayo mara nyingi wanaziweka kama ni fedha za miradi ya maendeleo, lakini kimsingi pesa zile zilitakiwa ziwe kwenye matumizi ya kawaida kwa sababu, zinaenda kuwasaidia vijana wetu pesa za kujikimu. Hii imekuwa ni mapendekezo ya Kamati mbalimbali, ikiwepo Kamati ya Bajeti.

Je, ili kuitendea haki Wizara hii kwa nini hizi pesa za mikopo msiziweke kwenye matumizi ya kawaida ili sasa tujue, kama Bunge, tuna jukumu gani la kutenga pesa za kutosha kwenye miradi ya maendeleo iende kwenye utekelezaji? Ahsante.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Ester Bulaya, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa vile hili ni wazo la Mheshimiwa Mbunge na amesema kwamba, ni mapendekezo ambayo yalitolewa na Kamati mbalimbali, sisi kama Wizara tutaenda kukaa na Wizara ya Fedha kuweza kuona namna gani jambo hili linaweza kwenda kufanyiwa kazi, lakini kimsingi tunaomba tulibebe. Ahsante.

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani mahsusi wa kuhakikisha vijana wote wanaoomba mikopo ya Elimu ya Juu wanapata mikopo hiyo kama walivyoomba?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Kwa kuwa mitaala pamoja na mikopo huzalisha wahitimu na kwa sababu, Wizara hii ndio Wizara ya kisera. Kwa mujibu wa taarifa ambayo ilitolewa hapa Bungeni na Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa mwaka, kati ya ajira zilizoombwa za ualimu elfu 10, walioajiriwa kama elfu 10, lakini waombaji walikuwa zaidi ya laki moja. Maana yake ni kwamba, ukiangalia mpaka waliohitimu mwaka jana ukijumlisha pale ni zaidi ya laki moja wako mtaani hawajapata ajira. Sasa swali langu, ni kwa nini Serikali au Wizara hii wasijadili hili suala la ajira ili kuwasaidia, hasa Walimu ambao ni Walimu wa Kiswahili, waende kufundisha Kiswahili kwenye nchi za Afrika Mashariki pamoja na SADC?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu swali dogo la Mheshimiwa Kakunda, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la ajira ni suala ambalo ni mtambuka na kwa vile Mheshimiwa Mbunge anatoa pendekezo kwamba, tuweze kuangalia namna gani tunaweza tukawasaidia Walimu kwenda kufundisha kwenye nchi hizi za Afrika Mashariki na Kati na Kusini mwa Afrika, tunaomba vilevile suala hili tulichukue, twende tukaangalie hizo fursa ambazo zinatokea kwenye nchi hizo na namna gani tunaweza tukakaa kitako na kuweza kushawishi namna gani Walimu wetu ambao wamehitimu kwenye shahada mbalimbali za ualimu, hasa hizi za Kiswahili kwenye vyuo vyetu, wanaweza kwenda kutumika kwenye maeneo hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, tunajua kwamba, masuala ya ajira mara nyingi sana yana-competition zake kwa sababu itakwenda kwenye usaili na watahitajika kwenda kwa ajili ya usaili huo. Kwa hiyo, hatuwezi kutoa guarantee moja kwa moja kwamba, tutafanya hivyo kwa asilimia 100, lakini nimwondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge, kwamba tunalichukua, tutaenda kulifanyia kazi na kuweza kuangalia namna gani nafasi hizo zinapatikana na tunaweza kunufaika sisi kama nchi.

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani mahsusi wa kuhakikisha vijana wote wanaoomba mikopo ya Elimu ya Juu wanapata mikopo hiyo kama walivyoomba?

Supplementary Question 4

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona na kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Katika uendelezaji wa sekta ya afya pamoja na sekta nyingine kuna watumishi ambao wanahitajika sana sasa hivi, kwa mfano clinical officers, wafamasia na hawa hawasomi vyuo vikuu. Kumekuwa na pendekezo la muda mrefu sana la kutoa mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vya kati ambalo ni hitaji kubwa sana katika nchi yetu kwa sasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali sasa ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba, wanafunzi wanaosoma vyuo vya kati pia wanapata mikopo kwa sababu, ndio mahitaji makubwa katika nchi yetu kulingana na miundombinu tunayoijenga kwenye maeneo ya vijijini ambayo yanahitaji sana hiyo kada ya kati kulitumikia Taifa? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mbunge wa Kilolo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli analozungumza Mheshimiwa Mbunge kwamba, uhitaji uko mkubwa sana kwenye vyuo vyetu vya kati, lakini kama tunavyofahamu na kama nilivyoeleza kwenye majibu ya swali la msingi, jambo kubwa hapa ni suala la bajeti. Iwapo kama bajeti yetu inaruhusu tunaweza tukavifikia vyuo vikuu vyote, lakini vilevile pamoja na vyuo vya kati. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge, bajeti itakaporuhusu tutahakikisha tume-cover kwanza eneo lote la vyuo vikuu halafu tutaangalia namna gani sasa mikopo hii inaweza kwenda kuwafaidisha au kuwanufaisha wenzetu wale ambao wako katika vyuo vya kati. Ahsante sana.

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani mahsusi wa kuhakikisha vijana wote wanaoomba mikopo ya Elimu ya Juu wanapata mikopo hiyo kama walivyoomba?

Supplementary Question 5

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kuniona ili niulize swali moja la nyongeza. Kwa kuwa katika majibu yaliyotolewa ya swali la msingi imeonekana changamoto kubwa ni ufinyu wa bajeti kwa mwaka hadi mwaka, pamoja na ongezeko la bajeti tuliyoelezwa, lakini ni ukweli kwamba, wanafunzi wenye sifa wanakuwa wengi na wale wanaokosa nafasi katika mwaka husika wengine wamekuwa wana kiu ya kuendelea na wananchi wamekuwa wakiwasaidia au jamii wanayoishi, sasa wakienda mwaka wa pili na watatu wanaendelea kukosa. Je, Serikali haioni inayo kila sababu sasa katika miaka inayofuatia wale wanafunzi waliosaidiwa katika njia mbalimbali wawaingize katika mwaka wa pili kabla hawajaendelea kuwachukua wengine?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Kibamba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba, utaratibu huo upo. Sio kwamba, ukikosa mkopo katika mwaka wa kwanza basi unakuwa hu-qualify kwenye mwaka wa pili, provided ulikuwa umeomba katika ule mwaka wa kwanza. Unachofanya katika ule mwaka wa pili, unakuwa wewe sio mwombaji mpya, unakuwa uko katika dirisha la rufaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, utaratibu huo upo Mheshimiwa Mbunge na tumekuwa tukiufanya na wanafunzi hao wamekuwa wakiwa-absorbed wakati wako mwaka wa pili ikiwa mwaka wa kwanza amekosa au mwaka wa tatu, hali ya mwaka wa kwanza na wa pili akiwa amekosa. Kwa hiyo, nikutoe wasiwasi na jambo hili tutaendelea nalo na ndivyo lilivyo.

Name

Tabasamu Hamisi Hussein Mwagao

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sengerema

Primary Question

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani mahsusi wa kuhakikisha vijana wote wanaoomba mikopo ya Elimu ya Juu wanapata mikopo hiyo kama walivyoomba?

Supplementary Question 6

MHE. TABASAM H. MWAGAO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Nasema usajili wa shule zetu, shule za msingi, sekondari na hadi vyuo vya kati hivi kama VETA, kumekuwa na masharti magumu sana katika Wizara ya Elimu. Kinachonishangaza hata shule za Serikali na zenyewe zinawekewa masharti magumu kupita kiasi, inatufanya sisi Wabunge ambao tuko vijijini huku wananchi wetu wanataka elimu, lakini tunapata zuwio kutoka katika Wizara ya Elimu.

Je, nini mpango wa Wizara ya Elimu kurahisisha usajili ili watu wengi waweze kusajili vyuo, kusajili shule zetu za msingi na sekondari? Ahsante.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Tabasam, Mbunge wa Sengerema, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Tabasam anazungumzia suala la usajili. Niwatoe wasiwasi Waheshimiwa Wabunge, suala la usajili wa shule au taasisi hizi, linaanzia kule ambako shule ipo. Tuna watumishi wetu, wataalam wetu ambao wako kwenye maeneo hayo katika wilaya ambao wanakwenda kufanya ukaguzi kwenye maeneo hayo. Baada ya ukaguzi huo mara nyingi sana huwa wanaandika taarifa, ili kuweza kuangalia ile miundombinu wezeshi kwa ajili ya kuanza kutoa elimu kama imefikiwa, basi tuweze kufanya hivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimtoe wasiwasi vile vile Mheshimiwa tabasam, hivi sasa Wizara iko mbioni kuhakikisha inakamilisha mfumo wa kufanya usajili kwa kupitia mfumo badala ya huu wa sasa wa kutumia makaratasi. Katika mfumo huo tunadhani vitu vingi sana vitakuwa ni rahisi na vyepesi na vitaondoa sana manung’uniko na mizunguko ile ambayo ilikuwa haina tija.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, katika kipindi hiki kifupi, tuendelee tu kuchukua hili wazo lake, lakini nimtoe wasiwasi, nakumbuka jana tulionana na nikamwambia leo tuonane tuweze kuangalia hayo maeneo yake ambayo anaona yana changamoto, lakini utaratibu kimsingi uko hivyo ni vitu tu vya kufuata utaratibu na fomu zile za kujaza. Tunaangalia zile requirements au yale mahitaji muhimu kwa ajili ya kuanza kutoa elimu kwa sababu, hatuwezi tu kusajili shule kwa sababu iko chini ya mti, ni lazima taratibu na miundombinu wezeshi iwepo. Hata hivyo, tunabeba wazo lake, tutakwenda kufanya maboresho kwenye eneo hili, lakini kwa vile mfumo unakwenda kuanza kufanya kazi, tunaamini maeneo mengi yatakwenda kuboreshwa. Ahsante sana.