Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza: - Je, ni Mikoa ipi inaongoza kwa mafanikio katika kampeni ya kuwabadili wakulima kutoka kwenye kilimo cha kujikimu na kulima kibiashara na ni mikoa ipi bado inasuasua?

Supplementary Question 1

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Jina langu ni Shally Josepha Raymond. Namshukuru Mungu sana kwa nafasi hii ya kupatiwa majibu haya mazuri na Serikali na nikuombe sasa niulize maswali yangu mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa katika jibu la msingi Mheshimiwa Naibu Waziri amenieleza wazi, kuwa sasa hivi wakulima wanalima kutokana na wao wenyewe walivyoamua. Maamuzi hayo ni mazuri sana, lakini swali langu la kwanza la msingi; kwa kuwa Serikali imeamua sasa kila mazao yanayolimwa yawe zaidi kibiashara na nchi hii utakuta kwamba shida kubwa ni mbegu. Wakulima wako tayari kulima sasa hasa mazao ya mbogamboga na TAHA iko kazini masaa 24 kutoa msaada kwa wakulima wa mbogamboga. Je, Serikali iko tayari sasa kutoa ruzuku kwa mazao hayo yakiwemo maparachichi, alizeti, mbogamboga zozote ambazo zinalimwa? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, wanawake wa Kilimanjaro wako tayari kulima kwenye vihamba vyao na Taasisi za Kilimanjaro za elimu, yakiwemo mashule yana mashamba ambayo yanalimwa mara moja tu mahindi lakini mwaka wote mzima yanakuwa hayana kitu. Je, Serikali iko tayari sasa kuwasaidia wakulima hao na wakina mama wa Kilimanjaro, kulima maparachichi kwa wingi na Taasisi hizo kuchimbiwa mabwawa ili mashamba yale yasikae idle mwaka mzima? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Shally Josepha Raymond, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza la kuhusu mbegu na ruzuku, ushauri huo tumeupokea tutakwenda kuufanyia kazi. Isipokuwa tu nataka nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba tumeendelea kukiimarisha Kituo chetu cha Utafiti wa Kilimo kwa maana ya (TARI). Hata ukiangalia bajeti imeendelea kuongezeka kwa sababu tunataka tufanye utafiti wa mbegu bora na zenye tija, ili mkulima wa Tanzania anufaike na kilimo kiwe cha tija.

Kwa hiyo, nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge ya kwamba eneo hili pia tumelipa kipaumbele na tunaendelea kuhakikisha kwamba, TARI inajengewa uwezo ili kuja basi na tafiti ambazo zitatusaidia katika kilimo bora.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la pili la kuwasaidia katika eneo la maparachichi hasa katika Taasisi zenye mashamba ambayo hayatumiki muda wote. Kama nilivyosema dhamira ya Serikali katika sekta ndogo hii ya kilimo cha mazao ya bustani na mbogamboga ni kuhakikisha tunaipeleka mbele parachichi. Kwanza kwenye kuongeza uzalishaji wetu kwa sababu hivi sasa kama nchi tunazalisha tani 48,000 kwa mwaka. Lakini lengo letu ni kwamba ifikapo mwaka, 2025 tufikishe tani 140,000 ya parachichi na tuongeze pia ku-export parachichi nje ya nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ili hayo yote yaweze kutokea lazima tuweke mkazo mkubwa kuhakikisha kwamba tunasaidia kilimo hiki kukua. Hivyo, kwa wanawake wa Kilimanjaro ambao Mheshimiwa Mbunge amewaulizia swali hili, nataka tu nimwahidi ya kwamba, mimi niko tayari kuandaa ziara maalum katika maeneo yote ambayo umeyataja, tuyapitie kwa pamoja na vile vile tuimarishe vituo vyetu ili mpate miche ya kutosha, basi waweze kulima parachichi kwa sababu soko limeshakuwa kubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza: - Je, ni Mikoa ipi inaongoza kwa mafanikio katika kampeni ya kuwabadili wakulima kutoka kwenye kilimo cha kujikimu na kulima kibiashara na ni mikoa ipi bado inasuasua?

Supplementary Question 2

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kuuliza swali dogo la nyongeza ambalo limejikita kwenye sekta hii hii ya zao la parachichi.

Nilisimama Bungeni hapa nikaomba kuhusu ugawaji wa miche ya parachichi kwa wakulima wetu. Kwa sababu, wakulima wetu wa Mkoa wa Njombe, Mkoa wa Mbeya, Mkoa wa Iringa wamejiwekeza sana kwenye kilimo cha parachichi, tukasema, kama ambavyo Serikali imefanya kugawa miche bure ya michikichi, miche bure ya pamba, miche bure ya korosho ili ku-boost wakulima wa mazao hayo, nikaiomba Serikali kuona ni mkakati upi ufanyike kwenye zao la parachichi ambapo wakulima wengi hawana fedha za kununua miche, lakini ni zao linaloonekana ni dhahabu ambalo sisi tunaita dhahabu ya kijani Mkoa wa Njombe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu, je, Serikali ina mkakati upi wa kuandaa vitalu ili iweze kugawa miche bure kwa wakulima ku-boost zao hili, kutoka kwenye kilimo cha kawaida kwenda kwenye zao la biashara ambalo kwa sasa ni hot kwenye Taifa letu? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kwanza nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu aliyoyatoa ya ufasaha. Nataka nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Festo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba Serikali imetoa ruzuku katika miche ya kahawa, tumetoa ruzuku katika miche ya korosho. Nataka nilihakikishie Bunge lako Tukufu kwamba sasa hivi Serikali inafanya mapping katika mikoa mitano, inayozalisha parachichi na kwa kutumia Taasisi zetu za TARI na TOSCI, tumeanza kutengeneza Regulation na Standardization ili kuondoa tatizo la miche inayouzwa na kila mwananchi barabarani ili tusije tukaua zao la parachichi na hivi karibuni tuta-launch hizo guideline. Tunaanza programu kupitia private sector partnership kama Serikali kuanzia mwaka ujao wa fedha. Tutazalisha miche, tutagawa kwa subsidized rate kwa sababu sasa hivi najua wakulima wananunua kati ya shilingi 5,000 na shilingi 6,000 kwa mche mmoja ambao ni ghali sana. Kwa hiyo, tutaanza kugawa miche ya ruzuku ya parachichi katika mikoa yote inayolima parachichi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la pili tutakalofanya kama Serikali katika eneo la parachichi ni kwamba, kama alivyosema Mheshimiwa Naibu Waziri, tutajenga common use facility tatu, moja tutaiweka kati ya Iringa na Njombe nyingine tutaiweka Dar es Salaam na nyingine tutaiweka Mkoa wa Kilimanjaro. Hizi zitatumika, wale wanunuzi wanaotoka nje watanunua parachichi, watafika katika hizo facility, watapata huduma kwa kuzilipia na zitawekwa alama ya kwamba ni product za Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu umwagiliaji. Timu yetu ya Umwagiliaji sasa hivi inafanya mapping katika mikoa hiyo ili tuone ni wapi ambapo tutaweza ku-facilitate kuweza kugawa mipira na nini ambako wananchi wamewekeza. Kwa sababu ni zao ambalo linahitaji uwekezaji wa muda mrefu na linahitaji government intervention, niwahakikishie tu Waheshimiwa Wabunge tutafanya strong intervention kwenye parachichi kwa sababu tunaamini tunazo competitive aids zote. (Makofi)

Name

Humphrey Herson Polepole

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza: - Je, ni Mikoa ipi inaongoza kwa mafanikio katika kampeni ya kuwabadili wakulima kutoka kwenye kilimo cha kujikimu na kulima kibiashara na ni mikoa ipi bado inasuasua?

Supplementary Question 3

MHE. HUMPHREY H. POLEPOLE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Tanzania ni mojawapo ya nchi mbili Ulimwenguni ambazo zimepewa baraka na Mungu ya kuzalisha organic phosphate. Organic phosphate ni mojawapo ya madini muhimu yanayotumika kutengeneza mbolea. Organic phosphate ulimwenguni inapatikana Tanzania na Australia peke yake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali, je, Serikali ina mpango gani wa kuzuia ku-export organic phosphate kama ambavyo inaendelea kufanyika sasa hivi, ili ibaki hapa nchini na kuendelea kuzalisha mbolea ili wakulima wetu wapate mbolea hapa na pasipo na kuhangaika kutoka maeneo mengine? Natambua kiwanda kinakuja Dodoma lakini kuna tamaa kubwa sana ya ku-export organic phosphate kwa sababu ni nchi mbili tu ulimwenguni ambazo zinatoa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Polepole, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kama nchi tunakuwa guided na WTO Regulation za Trade. Kwa hiyo, ku-declare openly tunazuia export au biashara yoyote sidhani kama katika misingi ya kibiashara ni jambo jema. Hilo la kwanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili sisi kama Serikali tumeshafanya comprehensive analysis kuangalia deposit yetu ya phosphate iliyopo katika nchi yetu. Tunazo taratibu za kuruhusu mahitaji yanapohitajika kwenda nje tunazo guidance zinazotu-guide. Haturuhusu export ya holela katika phosphate. Hilo la pili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la tatu kwa kuwa tumeshapata Mwekezaji ambaye anawekeza na atatumia phosphate katika Kiwanda cha Mbolea, kinachojengwa hapa Dodoma ambacho kinazalisha tani 600,000 na kitaanza mwaka kesho mwezi wa pili kuanza kuzalisha. Nataka niwahakikishie tu wakulima kwamba tuta-regulate matumizi ya rasilimali hii kwa maslahi ya Watanzania bila kuathiri mahusiano yetu ya kibiashara na nchi zingine. (Makofi)