Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 3 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 21 2022-02-03

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza: -

Je, ni Mikoa ipi inaongoza kwa mafanikio katika kampeni ya kuwabadili wakulima kutoka kwenye kilimo cha kujikimu na kulima kibiashara na ni mikoa ipi bado inasuasua?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo napenda kujibu swali la Mheshimiwa Shally Josepha Raymond, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kampeni ya kilimo biashara hapa nchini ilianza katika mazao yenye asili ya biashara ambayo ni pamoja na pamba, korosho, kahawa, pareto, chai, tumbaku na mkonge ambapo uhamasishaji wake ulifanyika kwa kuanzisha Vyama Vikuu vya Msingi vya Ushirika na Masoko (AMCOS).

Mheshimiwa Mwenyekiti, mikoa inayolima mazao ya kibiashara ni pamoja na Mwanza, Kagera, Geita, Shinyanga, Simiyu, Mara, Tabora, Kilimanjaro, Tanga, Pwani, Mtwara, Lindi na baadhi ya maeneo ya mikoa ya Arusha, Ruvuma, Mbeya, Songwe, na Iringa. Kufuatia kazi kubwa iliyofanywa na Wizara ya Kilimo kwa kushirikiana na wadau mbalimbali katika utoaji wa elimu ya kilimo biashara na utafutaji wa masoko ya mazao, wakulima katika mikoa hii wamebadilika na kwa sasa wanalima kilimo cha kibiashara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mikoa ambayo ilikuwa nyuma katika kutekeleza dhana ya kilimo biashara ilikuwa ni pamoja na mikoa ya Rukwa, Katavi, Kigoma, Dodoma, Singida, Morogoro, Manyara na Njombe. Mazao makuu katika mikoa hii ni yale ya nafaka, mikunde na mazao ya mafuta ambayo yalikuwa yakilimwa zaidi kwa ajili ya usalama wa chakula. Hivyo, kutokana na elimu ya kilimo biashara ambayo imekuwa ikitolewa kwa Maafisa Kilimo na wakulima katika mikoa hii, wakulima wengi wamebadilika na wanalima mazao kwa kuzingatia mahitaji ya soko.