Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Miraji Jumanne Mtaturu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mashariki

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU Aliuliza: - Je, Serikali ina Mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa skimu ya umwagiliaji Mang’onyi ili kuongeza tija ya kilimo cha mbogamboga kwenye Kata za Mang’onyi na Makiungu?

Supplementary Question 1

MHE. MIRAJI J. MTATURU: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nachukua nafasi hii kumshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mafupi ambayo bado hayajaondoa kabisa hamu ya wananchi wa Singida Mashariki kutumia banio hili. Kwa kuwa kilimo cha umwagiliaji kimeonekana ni kilimo chenye tija na hapa Bungeni tumekuwa tukizungumza mara kwa mara; na kwa kuwa soko la mbogamboga lipo kubwa sana kwenye mgodi wa Shanta Gold Mine pale Mang’onyi ambapo tunategemea utaanza hivi karibuni, ambalo litakuwa ni soko kubwa la mbogamboga na matunda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa Serikali haioni umuhimu wa sasa kutenga fedha ambazo zilikadiriwa shilingi milioni 580 ili kuweza kukamilisha upande uliobakia kumalizia banio hilo lililokuwa limeandaliwa? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Kwa kuwa chanzo cha maji na Bwawa la Mwiyanji alilolieleza limejaa tope na kusababisha maji kuwa siyo ya kutosha; na kwa kuwa tumekuwa tukipiga kelele kuhusiana na mabwawa hapa nchini yajengwe mengi ili kuongeza uwezo: Ni lini sasa Serikali itaweza kutenga fedha kwa ajili ya kuondoa tope za bwawa hilo la Mwiyanji ili liwe na kina cha kutosha na maji mengi na kuweza kujenga bwawa lingine ambalo litajengwa katika Kijiji husika cha Mang’onyi? Ahsante sana.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Miraji Jumanne Mtaruru, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kwanza na la msingi ni kwamba Serikali inatambua umuhimu wa kilimo cha umwagiliaji. Kwa kuwa kilimo hiki kinagusa pia sekta ndogo ya mbogamboga, Serikali itaendelea kuweka mkazo mkubwa kuhakikisha kwamba mradi huu unakamilika kwa hekta zilizobaki ili wananchi wa eneo la Mang’onyi waweze kupata huduma hii ya kilimo cha umwagiliaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hakika ni kwamba, katika bajeti inayokuja tutatenga fedha kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa mradi huu ili wananchi waweze kulima kupitia kilimo cha umwagiliaji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, ili mradi huu uweze kutekelezeka vizuri, na Mheshimiwa Mbunge bahati nzuri amelieleza jambo hili vizuri na amekuwa mtetezi wa kweli kwa wananchi katika jambo hili, lazima katika fedha ambazo zitatengwa zijumuishe pia namna ya kuweza kuondoa tope katika Bwawa la Mwiyanji ili maji yaweze kutiririka kwa urahisi ili wananchi waweze kupata huduma hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge nikuondoe hofu; pia mimi na wewe tumepanga kwamba baada ya hapa tutakwenda kutembelea na kuzungumza na wakulima ili kuona skimu nzima na kuona namna Serikali inaweza ikawasaidia kwenye skimu hiyi.

Name

Husna Juma Sekiboko

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU Aliuliza: - Je, Serikali ina Mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa skimu ya umwagiliaji Mang’onyi ili kuongeza tija ya kilimo cha mbogamboga kwenye Kata za Mang’onyi na Makiungu?

Supplementary Question 2

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Kwa kuwa Wilaya ya Lushoto ni maarufu sana kwa kilimo cha mbogamboga na matunda, lakini kilimo hicho kimeendelea kusuasua kutokana na kilimo hicho kutegemea zaidi mvua za asili: -

Je, ni lini sasa Serikali itaandaa mpango wa kuvuna maji ya mvua ili baadaye yaweze kutumika katika umwagilia kipindi hicho cha ukame?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Husna Sekiboko, Mbunge wa Viti Maalum, kutoka Mkoa wa Tanga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni dhahiri kwamba ili kilimo chetu kiweze kuendelea, hatupaswi kuendelea tena kutegemea maji ya mvua. Kwa hiyo, kilimo cha umwagiliaji ndiyo tiba na ndiyo mwarobaini wa changamoto tuliyonayo. Kwa wakulima wa Lushoto, kazi inayofanyika pale kubwa ni lazima kuwajengea uwezo kwa kuhakikisha kwamba wanapata skimu hizo za umwagiliaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri wa Kilimo pamoja na Waziri wa Fedha wiki mbili zilizopita walifanya mkutano pamoja na Benki ya BADEA kwa ajili ya kupata mkopo wa kuja kujenga skimu kubwa za umwagiliaji ambazo zitasaidia sana kutatua changamoto katika maeneo mengi ndani ya nchi hii. Hivyo Waheshimiwa Wabunge tuendelee kuiunga mkono Wizara yetu katika hatua ambayo tumefikia, basi fedha hizo za BADEA zikipatikana tuweze kujenga miradi mingi na mikubwa katika nchi yetu ili kilimo cha umwagiliaji kiweze kupata nafasi yake.

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU Aliuliza: - Je, Serikali ina Mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa skimu ya umwagiliaji Mang’onyi ili kuongeza tija ya kilimo cha mbogamboga kwenye Kata za Mang’onyi na Makiungu?

Supplementary Question 3

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Zipo skimu zilizoanzishwa na Serikali ikiwemo skimu ya Karema ambayo ilianzishwa toka miaka iliyopita kama saba hivi. Skimu hiyo haijafanya kazi na zipo nyingi nchini zinazofanana na ile skimu: -

Je, ni lini Serikali itakwenda kukamilisha miradi iliyoanzishwa huko nyuma ukiwemo mradi wa skimu ya Karema?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Kakoso, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri wa Kilimo ameshatoa maelekezo kwa Tume ya Umwagiliaji Nchini kwa kuhakikisha ina take stock ya scheme zote nchini kwa zile zinazofanya kazi na ambazo zinahitaji ukarabati na zile ambazo zinahitajika kujengwa mpya. Hivi sasa kazi hiyo inaendelea na katika maeneo hayo pia tutaigusa skimu hiyo ambayo Mheshimiwa Mbunge ameisema ya Karema; na tutatoa pia maelezo ndani ya Bunge letu hatua ambazo tumezifikia kwa ajili ya utekelezaji wa miradi hii mikubwa.

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU Aliuliza: - Je, Serikali ina Mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa skimu ya umwagiliaji Mang’onyi ili kuongeza tija ya kilimo cha mbogamboga kwenye Kata za Mang’onyi na Makiungu?

Supplementary Question 4

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuuliza swali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Hai kwa asilimia 78 tunategemea kilimo cha umwagiliaji, lakini pia tunazo skimu
25 za kimkakati ambazo tukizitumia tutabadilisha kabisa maisha ya watu na sisi kushiriki katika pato la Taifa. Tarehe 21Januari, 2022 Mheshimiwa Rais akiwa anaelekea Moshi Mjini alisimama pale Bomang’ombe, nami nilipata nafasi ya kumwomba atujengee skimu hizi. Alituahidi atatujengea kwa kutambua umuhimu mkubwa wa skimu hizi.

Swali langu, ni lini sasa Serikali itatekeleza agizo la Mheshimiwa Rais? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Saashisha Mafue, Mbunge wa Hai kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahadi ya Mheshimiwa Rais ni maelekezo kwetu na tumeipokea na tutaitekeleza kwa kadri ambavyo fedha zitaruhusu, kuanzia mwaka ujao wa fedha. Kwa hiyo, nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba tumepokea ahadi ya Mheshimiwa Rais na tutaitekeleza kadri ambavyo fedha zitakuwa zinapatikana ndani ya Wizara.

Name

Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU Aliuliza: - Je, Serikali ina Mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa skimu ya umwagiliaji Mang’onyi ili kuongeza tija ya kilimo cha mbogamboga kwenye Kata za Mang’onyi na Makiungu?

Supplementary Question 5

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Kama nchi, ni muhimu kuwa na zao la kimkakati ambalo tuna uhakika wa kutupatia fedha za kigeni. Sasa kwenye zao la mbogamboga, horticulture hususan parachichi, sasa hivi kila mtu anajua kwamba kuna demand kubwa sana ya parachichi duniani na tafiti zilizofanyika karibuni, zinaonesha kwamba Tanzania ni kati ya nchi ambazo zinatoa parachichi bora kabisa duniani. Sasa kuna mikoa ambayo inalima parachichi, lakini ina mabonde ya asili yenye maji; ukizungumzia Njombe, Mbeya, Iringa, baadhi ya maeneo ya Songea na Songwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu kwa Serikali, kwa kuzingatia maeneo haya yana mabonde ya asili, maji yanapatikana kiurahisi sana; kwa nini kusiwe na mkakati mahsusi, ukizingatia demand kubwa ya parachichi duniani, haya mabonde yakaendelezwa kwa gharama nafuu, wananchi wakapata maji, kwa sababu parachichi ili liwe bora linahitaji maji na mbolea ili wananchi wapate na Serikali ipate: Sasa nataka majibu, katika hiyo mikopo ambayo mnasema mnazungumza, kuna mikakati gani mahususi ya kuendeleza mikoa hii mitano ili wakulima wanufaike na Serikali inufaike? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali ya Mheshimiwa Halima Mdee, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika sekta ndogo ya mazao ya mbogamboga na bustani, moja kati ya zao ambalo tumelipa kipaumbele kama Wizara hivi sasa ni zao la parachichi, kwa sababu tunatambua ya kwamba hivi sasa soko lake ni kubwa. Pia tumeshafungua masoko ya parachichi katika nchi za India pamoja na Afrika ya Kusini huku mawasiliano na majadiliano yakiendelea katika nchi za China na Marekani. Kwa kutambua umuhimu huo, katika mkopo huu ambao nimeuzungumza, moja kati ya maeneo ambayo yatakwenda kuguswa pia ni maeneo ambayo yanagusa mikoa hii ili kuhakikisha ya kwamba zao hili linapata huduma stahiki kutokana na upatikanaji wa maji mengi ya kutosha na pembejeo ya mbolea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lengo letu kubwa katika hili ni kuifanya Tanzania ijulikane kwa parachichi kama zao la kipaumbele. Hatua ambazo zimeshachukuliwa kwa hivi sasa ni kwamba Mheshimiwa Waziri ameshatoa maelekezo ya ujenzi wa common use facility katikati ya mikoa ya Mbeya na Iringa ambayo itasaidia kulima parachichi yetu kwa ufasaha. Vile vile parachichi itakayovunwa itapelekwa kwenye park moja ambayo tutafanya sorting, grading na packaging na kuifanya parachichi yetu ni produce of Tanzania kuliko hivi sasa ambapo parachichi yetu katika baadhi ya maeneo inaonekana kama inatoka nje ya nchi ya Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hii ni hatua kubwa ambayo tumeichukua katika hatua ya awali kabisa, lakini lengo letu kubwa kabisa ni kuhakikisha kwamba tunaendelea kufungua masoko ya parachini lakini vilevile kuwajengea wakulima uwezo na kulipa kipaumbele zao la parachichi. (Makofi)