Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 3 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 20 2022-02-03

Name

Miraji Jumanne Mtaturu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mashariki

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU Aliuliza: -

Je, Serikali ina Mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa skimu ya umwagiliaji Mang’onyi ili kuongeza tija ya kilimo cha mbogamboga kwenye Kata za Mang’onyi na Makiungu?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO Alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu leo ni mara yangu ya kwanza kusimama hapa, napenda nichukue fursa hii kwanza kabisa kumshukuru Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema aliyeniwezesha kufika siku ya leo na kwa Ukuu wake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, nachukua fursa hii kumshukuru sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa imani yake kubwa kwangu na kuahidi kwamba nitailinda imani hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Miraji Jumanne Mtaturu, Mbunge wa Singida Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Skimu ya Mang’onyi ambayo ipo Mkoani Singida imeendelezwa kwa kujengewa banio linalopokea maji kutoka Bwawa la Mwiyanji na takribani hekta 50 kati ya hekta 450 zimeendelezwa kwa kujengewa miundombinu ya umwagiliaji na sehemu ya shamba lililobaki hufikiwa na maji kwa njia ya asili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea kutafuta fedha ili kukamilisha ujenzi wa Skimu ya Mang’onyi.