Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maryam Azan Mwinyi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI aliuliza: - Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwapatia wavuvi elimu ya uelewa kuhusu madhara ya uvuvi haramu ili wasifanye aina hiyo ya uvuvi na kuharibu mazingira ya maziwa na bahari nchini?

Supplementary Question 1

MHE. MARYAM AZAN MWINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa vile Serikali imetoa majibu mazuri sana, naomba kuuliza swali moja la nyongeza.

Je, Serikali imefanya tathmini katika elimu inayotoa, kama kusaidia kupunguza uvuvi huu haramu ambao bado tunauona unaendelea?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge Maryam Azan Mwinyi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati wote tumekuwa tukifanya tathmini na ninakubaliana na Mheshimiwa Mbunge ya kwamba pamoja na elimu tunayoitoa, bado tatizo la uvuvi haramu liko pale pale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndani ya Serikali tumekubaliana; la kwanza, elimu ni jambo endelevu, kwa hiyo, tutaendelea nalo. La pili, ni kupanua wigo na kufanya ushirikishaji zaidi ili kusudi tuweze kupambana na vita hii ya uvuvi haramu kwa pamoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nikuhakikishie ya kwamba wavuvi walio wengi wanaelewa sana ya kwamba hiki ni sahihi na kipi kisicho sahihi. Tunazo changamoto za msingi sana ambazo zinawapelekea wakati mwingine baadhi yao; aidha kwa makusudi au kwa au kwa bahati mbaya wanaingia katika vitendo hivi haramu. Miongoni mwa changamoto hizo ni ongezeko la mahitaji ya hizi rasilimali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge ya kwamba Serikali tunafanya tathmini na tunaendeleza mikakati ya kuhakikisha tunafanya uendelevu wa rasilimali zetu.

Name

Angelina Adam Malembeka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI aliuliza: - Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwapatia wavuvi elimu ya uelewa kuhusu madhara ya uvuvi haramu ili wasifanye aina hiyo ya uvuvi na kuharibu mazingira ya maziwa na bahari nchini?

Supplementary Question 2

MHE. ANGELINA A. MALEMBEKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Mheshimiwa Waziri ameelezea jinsi gani walivyojipanga kutoa elimu ya kuondoa madhara ya uvuvi haramu; na mara nyingi uvuvi haramu hufanyika kwa vifaa duni na ambavyo siyo sahihi; na vifaa sahihi hupatikana kwa gharama kubwa; na wengi wanaofanya uvuvi haramu ni kwa sababu hawana vifaa vile: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitaka kujua: Je, Serikali ina mpango gani ili kuinua kundi hili la wavuvi wadogo wadogo kiuchumi hasa katika Pwani yetu ya Bahari ya Hindi na Maziwa Makuu? Ahsante.

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Angelina Malembeka kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpongeze sana kwa kuwa amekuwa kila mara mstari wa mbele kwenye kuwasemea wavuvi hasa wavuvi wadogo wadogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya pongezi hizi, ni kwamba mkakati wetu ni kuendelea kurekebisha sheria zetu na kuziboresha. Hili ni jambo la kwanza ili kusudi ziweze kuendana na wakati, maana wavuvi wamekuwa kila mara wanagundua zana mpya, zana ambazo labda wakati mwingine kwa upande wa sheria zetu tunakuwa nyuma ya teknolojia hizi ambazo wavuvi wamezigundua. Kwa hiyo, huu ni mkakati wetu wa kuhakikisha tunakwenda nao sambamba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili ni kurekebisha katika masuala ya kikodi. Tumekuwa tukifanya hivyo kila mara ili zana zetu ziweze kukidhi haja ya wavuvi kwa maana ya bei; na tatu ni mkakati wetu wa kuunda vikundi vya ushirika wa wavuvi na waweze kupata mikopo iliyo na riba nafuu kupitia Benki yetu ya Kilimo na hatimaye kuweza kuwasaidia kwenye kufanya shughuli zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nne, naomba niwaambie Waheshimiwa Wabunge, tunayo dhana pana sasa ya uchumi wa blue ambayo tumedhamiria, Serikali ya Awamu ya Sita ya Rais Samia Suluhu Hassan kuhakikisha kwamba tunahamasisha na kutangaza dhana hii ambapo katika ukanda wote mathalan wa bahari ya hindi tuweze kutumia ipasavyo rasilimali zote zinazopatikana ili kuweza kuwafanya wavuvi wetu wawe na kipato kinachotosheleza kwa ajili ya kaya kwa maana ya familia zao na kuweza kuwa na mchango mpana kwenye pato la Taifa letu.

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI aliuliza: - Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwapatia wavuvi elimu ya uelewa kuhusu madhara ya uvuvi haramu ili wasifanye aina hiyo ya uvuvi na kuharibu mazingira ya maziwa na bahari nchini?

Supplementary Question 3

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa Wizara tayari imeshaanza utaratibu wa kutoa elimu ya huo uvuvi unaoitwa haramu, miongoni mwa wilaya zilizoathirika ni pamoja na Wilaya ya Nkansi ambao walichomewa nyavu zao kwamba wanavua uvuvi haramu, lakini Serikali haijawahi kuwapatia mbadala wa nyavu zinazoitwa halali. Leo wamejikongoja wachache wameendelea na uvuvi, wanavamiwa na watu kutoka Kongo na Burundi. Wajibu wa Wizara ni kuwalinda wavuvi hawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kujua, mna mkakati gani wa haraka wa kuwasaidia wavuvi hawa ambao wamevamiwa na vifaa vyao bado viko Kongo na Burundi?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Aida Khenani, Mbunge wa Nkansi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo hili ni jinai na kwa hiyo, litashughulikiwa katika utaratibu wa kijinai. Naomba kwa kuwa ni jambo mahususi, tuweze kushughulika nalo katika utaratibu wake. Hapa umetaja nchi ambazo ni majirani zetu. Kwa hiyo, unaweza ukaona kwamba ni jambo mtambuka. Hapa umetaja jambo ambalo linaweza kushughulikiwa pia na Wizara, sisi na Wizara ya Mambo ya Ndani ya na kwa sababu linahusisha nchi nyingine na Wizara ya Mambo ya Nchi na Nje na wengine tunaohusika katika masuala ya ulinzi na usalama wa Taifa letu. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI aliuliza: - Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwapatia wavuvi elimu ya uelewa kuhusu madhara ya uvuvi haramu ili wasifanye aina hiyo ya uvuvi na kuharibu mazingira ya maziwa na bahari nchini?

Supplementary Question 4

MHE. JACKSON G. KISWAGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa uvuvi haramu umeathiri sana mapato hasa kwenye mabwawa mengi, pamoja na Bwawa la Mtera ambapo Halmashauri ya Iringa Vijijini imekuwa ikipata mapato yake.

Je, Serikali ina mpango gani wa kutengeneza mabwawa yawe mashamba darasa kwenye Halmashauri nyingi pamoja na Jimbo la Kalenga ili tuweze sasa kufundisha vijana wengi pamoja na akinamama na akinababa waanze kutegemea uchumi wa kufuga samaki kupitia haya mabwawa ambayo yatakuwa ni mashamba darasa? Ahsante sana.

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kiswaga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunao mkakati wetu. Katika bajeti ya mwaka huu 2021/2022 kupitia mradi wa AFDP kwa maana ya Agricultural Fisheries Development Program II, tumetenga pesa kwa ajili ya kuweza kutengeneza mashamba darasa ya ufugaji wa Samaki. Hapa walengwa ni makundi ya vijana na akina mama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimkaribishe Mheshimiwa Kiswaga ili tuweze kushirikiana katika hatua hii. Yawezekana Wilaya ya Iringa Vijijini kwa maana ya Jimbo lake likawa ni sehemu ya wanufaika. Ahsante sana. (Makofi)