Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 2 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 12 2022-02-02

Name

Maryam Azan Mwinyi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI aliuliza: -

Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwapatia wavuvi elimu ya uelewa kuhusu madhara ya uvuvi haramu ili wasifanye aina hiyo ya uvuvi na kuharibu mazingira ya maziwa na bahari nchini?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa fursa hii ya kujibu maswali, lakini kwanza naomba nami nimshukuru Mwenyezi Mungu; na pili, nimshukuru sana Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuniamini katika Wizara hii kwa nafasi hii ya Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya maneno hayo ya shukrani, naomba sasa kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri, kujibu swali la Mheshimiwa Maryam Azan Mwinyi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inakubaliana kabisa na Mheshimiwa Mbunge kuwa ni muhimu sana kuwapatia wavuvi elimu kuhusu madhara ya uvuvi haramu ili wasifanye uvuvi haramu na tuweze kulinda rasilimali za uvuvi nchini. Katika kutekeleza jukumu hili, Serikali imekuwa ikitoa elimu hiyo kupitia vipindi vya redio, runinga, mikutano, vipeperushi, semina na maonesho mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile wataalam wa Wizara wamekuwa wakitoa elimu kwa kuwafikia wavuvi na wadau wengine moja kwa moja katika maeneo yao ambapo kwa mwaka 2021/2022 mikoa ambayo tayari imefikiwa ni mikoa ya Tanga, Pwani, Mwanza, Mara, Kagera na Katavi. Ahsante sana.