Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jamal Kassim Ali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magomeni

Primary Question

MHE. JAMAL K. ALI aliuliza:- Kwa miaka mingi nyuma TANESCO ilikuwa ndicho chombo kilichohusika katika kuuza na kupanga bei za umeme kwa wateja wake katika makundi tofauti ya wateja wake katika nchi yetu mpaka pale EWURA ilipoanzishwa na kuanza kufanya kazi:- (a) Je, ni vigezo gani ambavyo EWURA inavitumia katika kupanga bei hizo? (b) Je, kuna unafuu gani wanaopata kwa wateja wanaochukua umeme katika mikondo mikubwa ya KV 11, KV 33 na KV 132?

Supplementary Question 1

MHE. JAMAL KASSIM ALI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri nitakuwa na maswali mawili madogo ya nyongeza.
Moja, kwa vile Mheshimiwa Naibu Waziri ameeleza kwamba kila mteja katika kila ngazi anabeba gharama zake. Je, Naibu Waziri atakubaliana nami kwamba bei ambayo inatozwa Shirika la Umeme la Zanzibar yaani ZECO, ambaye ni mteja wa jumla (bulk purchaser) kwa unity moja ya KVA ambayo ni shilingi 16,550/= ambayo ni bei kubwa kuliko wale wateja wa reja reja wa ngazi ya kati na ngazi ya chini kuwa hii bei siyo stahiki kutozwa ZECO. Je, lini Serikali itaitaka EWURA sasa kufanya maboresho ya bei hii na kuitoza ZECO bei stahiki? Ahsante.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa. Kwanza nimshukuru Mheshimiwa Jamali kwa kutukumbusha kwamba gharama za umeme zinatakiwa zishuke. Nimhakikishie tu kwamba kuanzia mwezi wa Nne tulipofanya marekebisho ya bei watumiaji wakubwa kabisa wakiwemo ZECO tuliwapunguzia kwa asilimia 2.4, ilikuwa ni punguzo kubwa kweli kweli ukilinganisha na wateja wengine wadogo wadogo. Kwa hiyo, namhakikishia Mheshimiwa Jamal kwamba bei za gharama kama nilivyosema, zinategemea hasa mambo mawili:-
Jambo la kwanza ni vyanzo vya kuzalisha umeme. Vyanzo vinapokuwa vya bei nafuu na bei ya umeme inapungua. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Jamal kwamba ni kweli kabisa kwa unity moja kwa sasa kwa watumiaji wakubwa ni shilingi 16 na 55 unit, lakini zitaendelea kupungua kulingana na gharama ya uzalishaji wa umeme unavyoshuka. Kwa hiyo, Mheshimiwa Jamal nakuhakikishia tutaendelea kulifanyia kazi na EWURA bado wanaendelea na mchakato wa ku-review bei kulingana na gharama za umeme.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili, ni lini sasa EWURA watafanya marekebisho hayo? Kwa sasa hivi tunazalisha umeme mwingi sana wa kutumia gesi na kwa kiasi kingine kikubwa kwa kutumia maji. Tumeeleza sana vyanzo vya gesi na jinsi ambavyo bei inaendelea kupungua. Kwa sasa hivi atupe muda tuendelee kuzalisha kwa vile ambavyo mmetupa bajeti, siyo muda mrefu, EWURA tena wataingia uwanjani kuanza ku-review bei. Kwa hiyo, Mheshimiwa Jamal nikuhakikishie kwamba bei itaendelea kuangaliwa wakati hadi wakati.

Name

Seif Khamis Said Gulamali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manonga

Primary Question

MHE. JAMAL K. ALI aliuliza:- Kwa miaka mingi nyuma TANESCO ilikuwa ndicho chombo kilichohusika katika kuuza na kupanga bei za umeme kwa wateja wake katika makundi tofauti ya wateja wake katika nchi yetu mpaka pale EWURA ilipoanzishwa na kuanza kufanya kazi:- (a) Je, ni vigezo gani ambavyo EWURA inavitumia katika kupanga bei hizo? (b) Je, kuna unafuu gani wanaopata kwa wateja wanaochukua umeme katika mikondo mikubwa ya KV 11, KV 33 na KV 132?

Supplementary Question 2

MHE. SEIF K. S. GULAMALI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza kwa Naibu Waziri. Kwa kuwa tatizo la umeme lililopo Zanzibar linafanana sana na tatizo la umeme lililopo Igunga, sasa kwa sababu Naibu Waziri anatambua vizuri sana: Je, nini kauli ya Serikali juu malipo ya fidia kwa Kata za Chabutwa, Simbo pamoja na Mwisi ili waweze hasa kujua watapata lini hiyo fidia yao? Ahsante.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Niabu Spika, kwanza namshukuru Mheshimiwa Gulamali, jana na juzi tumehangaikia sana suala la fidia ya wananchi wako. Kama ambavyo tumelifikisha, kwanza nikupongeze. Sasa hivi mthamini wa ardhi wa Mkoa anapitia viwango vya fidia vya wananchi wa Manonga na hasa katika vijiji vya Chabutwa Simbo na maeneo ya jirani ambapo umetaja, ni kweli kabisa kuna wananchi 722 ambao hawajafidiwa na malipo hayo yako katika hatua za mwisho.
Mheshimiwa Naibu Spika, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba jana wakati tunapitia, tulipoongea na Mkuu wa Mkoa wa Tabora nadhani alikwambia kwamba kabla ya mwezi ujao na miezi miwili ijayo wananchi wako watalipwa fidia. Kwa hiyo, nakuomba sana wafikishie taarifa waendelee kuwa na subira jambo la fidia yao linafanyiwa kazi.

Name

Salum Mwinyi Rehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Primary Question

MHE. JAMAL K. ALI aliuliza:- Kwa miaka mingi nyuma TANESCO ilikuwa ndicho chombo kilichohusika katika kuuza na kupanga bei za umeme kwa wateja wake katika makundi tofauti ya wateja wake katika nchi yetu mpaka pale EWURA ilipoanzishwa na kuanza kufanya kazi:- (a) Je, ni vigezo gani ambavyo EWURA inavitumia katika kupanga bei hizo? (b) Je, kuna unafuu gani wanaopata kwa wateja wanaochukua umeme katika mikondo mikubwa ya KV 11, KV 33 na KV 132?

Supplementary Question 3

MHE. SALUM MWINYI REHANI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri kuhusiana na bei ya umeme bado Shirika la Umeme la Zanzibar (ZECO) halijapunguza bei ya umeme kitu ambacho kinawanyima fursa wananchi wa Zanzibar kuweza kutumia nishati hii au rasilimali hii kwa ukubwa zaidi kuliko hali inavyokuweko sasa hivi. Kwa sababu wengine wanashindwa kuunga umeme kutokana na hali ya bei. Je, Serikali ina mpango gani wa kuweza kukaa na ZECO ili kuona na kwamba na wao viwango vile vinaweza kupungua na kuwanufaisha wananchi wote kwa bei ya chini zaidi kama ilivyokuwa huku Tanzania Bara.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa kule ZECO kama ambavyo mnajua, wanajua umeme wa jumla na kwa vile wananunua umeme wa jumla, siyo rahisi sana wakaona punguzo la bei ya umeme. Hata hivyo, nakubaliana na Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali iko tayari kukaa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar pamoja na ZECO, TANESCO na EWURA ili kuona ni jinsi gani sasa gharama za umeme zinaweza kupitiwa upya. Nitoe tu angalizo, gharama za umeme zinazingatia sasa vyanzo vyetu pamoja na gharama nyingine za uzalishaji.
Mheshimiwa Naibu Spika, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali iko tayari, tutakaa pamoja na wewe pamoja na EWURA ili pia kuangalia upya bei za umeme huko Zanzibar.

Name

Joram Ismael Hongoli

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. JAMAL K. ALI aliuliza:- Kwa miaka mingi nyuma TANESCO ilikuwa ndicho chombo kilichohusika katika kuuza na kupanga bei za umeme kwa wateja wake katika makundi tofauti ya wateja wake katika nchi yetu mpaka pale EWURA ilipoanzishwa na kuanza kufanya kazi:- (a) Je, ni vigezo gani ambavyo EWURA inavitumia katika kupanga bei hizo? (b) Je, kuna unafuu gani wanaopata kwa wateja wanaochukua umeme katika mikondo mikubwa ya KV 11, KV 33 na KV 132?

Supplementary Question 4

MHE. JORAM ISMAEL HONGOLI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuliza swali la nyongeza. Katika Jimbo la Lupembe, Kata ya Kidegembye tuna tatizo kubwa sana la umeme hasa tatizo la low voltage. Transformer iliyopo pale haiwezi kuzalisha umeme wa kutosha na hivyo kutoweza kusambaza umeme sehemu nyingi na wananchi wa pale hawawezi kufanya shughuli za kiuchumi kama vile welding na shughuli nyingine za kusaga nafaka. Je, ni nini kauli ya Serikali kutatua tatizo hili? Maana nimewaona watu wa TANESCO muda mrefu lakini mpaka leo hii tatizo hilo bado lipo.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa kama mlivyoona katika maeneo mengi, sasa hivi bado tunaendelea na harakati ya kusafirisha umeme wa msongo mkubwa wa Kilovolt 400.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema, Wizara yetu ina jumla ya miradi 42 sasa. Kati ya miradi 42, miradi 16 ni kwa ajili ya uzalishaji umeme wa gesi pamoja na usambazji wake; lakini miradi 11 ni kwa ajili ya miradi ya maji na kusambaza umeme wa maji. Miradi mingine minane ni kwa ajili ya vyanzo vingine na miradi saba ni rasmi kwa ajili ya usambazaji umeme mkubwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, tumekuwa tukisema sana kwamba kuanzia sasa Wakandarasi wako site na kazi kubwa hasa maeneo ya Iringa, Njombe Dodoma, Sumbawanga na mengine, tunaanza sasa mradi wa kusafirisha umeme wa Kilovolt 400. Kazi ya mradi huu kuongeza nguvu kubwa ili umeme sasa usiwe unakatikakatika.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa sasa hivi tunatumia umeme wa low voltage, lakini tutakapokamilisha miradi hii mwaka 2018/2019 low voltage sasa itakuwa imekwisha kwa sababu itakuwa na umeme mkubwa. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge wa Njombe pamoja na maeneo ya Lupembe na mengine ni kuhakikishie kwamba taratibu wa umeme kukatika zinachangiwa pia sasa na low voltage lakini kwa sababu tuna umeme mkubwa gharama hizo pia zitashuka lakini na umeme utakuwa haukatiki.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine, kama nilivyosema, maeneo mengine umeme unakatika siyo kwa sababu ya low voltage tu, ni kwa sababu ya miundombinu kuwa mibovu. Sehemu ya miundombinu ni pamoja na transformer.
Nawashukuru Waheshimiwa Wabunge, mmepitisha Sheria ya Manunuzi na tumeshasema, kuanzia sasa transformer tutakuwa tunanunua hapa nchini kwa sababu shirika letu na kampuni yetu ya TANELEC sasa itakuwa na uwezo wa kutosha wa kutengeneza transformer na Serikali itanunua, kwa hiyo, matatizo ya transformer yatarekebika na kupunguza kabisa tatizo la kukatika kwa umeme.