Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 54 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 464 2016-06-30

Name

Jamal Kassim Ali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magomeni

Primary Question

MHE. JAMAL K. ALI aliuliza:-
Kwa miaka mingi nyuma TANESCO ilikuwa ndicho chombo kilichohusika katika kuuza na kupanga bei za umeme kwa wateja wake katika makundi tofauti ya wateja wake katika nchi yetu mpaka pale EWURA ilipoanzishwa na kuanza kufanya kazi:-
(a) Je, ni vigezo gani ambavyo EWURA inavitumia katika kupanga bei hizo?
(b) Je, kuna unafuu gani wanaopata kwa wateja wanaochukua umeme katika mikondo mikubwa ya KV 11, KV 33 na KV 132?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Jamal Kassim Ali, Mbunge wa Magomeni, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Naibu Spika, EWURA hupanga bei ya umeme kwa kuzingatia gharama halisi za uendeshaji wa biashara kama ilivyobainishwa kwenye Sheria ya Umeme ya mwaka 2008. Bei hiyo ya umeme hupangwa kulingana na makundi ya watumiaji ili kila kundi libebe gharama zake.
(b) Mheshimiwa Naibu Spika, TANESCO ina wateja mbalimbali ikiwa ni pamoja na wateja wa majumbani ambao ni D1 na T1. Wateja wa viwanda vidogo vidogo ambao pia wanatumia msongo wa volti 400 na matumizi kwa mwezi ni zaidi ya uniti 7,500 ambao ni T2, lakini wateja wakubwa waliounganishwa katika msongo wa kati wa medium voltage yaani T3 na MV na wateja wakubwa waliounganishwa katika msongo mkubwa (high voltage: T3-HV).
Mheshimiwa Naibu Spika, unafuu wanaopata wateja wanaounganishwa katika msongo mkubwa wa umeme ni kuwa na bei ya chini (energy charge) ukilinganishwa na wateja wadogo, hasa majumbani ambao ni T1. Unafuu huo unatokana na ghrama za usambazaji na upotevu wa umeme kuishia kwenye mfumo wa HV na medium V, yaani kilovoti 220, Kilovoto 132, KV 66, KV 33 pamoja na KV 11.
Mheshimiwa Naibu Spika, kulingana bei za umeme zilizopo hivi sasa, mteja wa T1 analipa shilingi 292/= kwa unit moja; mteja wa viwanda vidogo vidogo (T2) wanalipa shilingi 195/= kwa unit moja na mteja wa T3-MV analipa shilingi 157/= kwa uniti moja; na mteja wa T3 yaani high voltage ikiwemo migodi mikubwa ya madini kama GGM na mingine, pamoja na ZECO wanalipa shilingi 152/= kwa unit moja.
Mheshimiwa Naibu Spika, h•Hata hivyo, wateja wadogo wadogo, hasa wa majumbani ambao ni D1 wanaotumia chini ya unit 75 kwa mwezi wanalipa shilingi 100/= kwa unit moja.