Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kavejuru Eliadory Felix

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Primary Question

MHE. KAVEJURU E. FELIX Aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kupanua Uwanja wa Ndege wa Kigoma ili Ndege kubwa ziweze kutua?

Supplementary Question 1

MHE. KAVEJURU E. FELIX: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza.

(a) Pamoja na mikakati ambayo Serikali imeionyesha je, ni lini sasa ujenzi huo utaanza? (Makofi)

(b) Kwa kuwa Mkoa wa Kigoma una Wilaya tatu mpya ambazo ni Buhigwe, Kakonko na Uvinza. Wilaya hizi hazina viwanja vidogo vya ndege. Serikali ina mkakati gani? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GEOFREY G. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Kavejuru amekuwa anafuatilia sana suala la ujenzi wa kiwanja hiki, lakini naomba tu nimtoe wasiwasi kwamba kwa maelewano ambayo yanaendelea, tunategemea tarehe 28 mwezi huu wa Pili, kupata Letter of No Objection na miradi yote hii minne tunaamini itaanza kutekelezwa. Hilo ni jibu la kwanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jibu la pili kuhusu ujenzi wa viwanja vya ndege vidogo ama air strip katika Wilaya za Buhigwe, Kakonko na Uvinza, hili litategemea na upatikanaji wa fedha kadri itakavyoruhusu, basi hivyo viwanja vinaweza vikajengwa. Ahsante. (Makofi)