Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA K.n.y. MHE. CHARLES M. KAJEGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza dhamira yake ya kuwatua Wanawake ndoo kichwani kwa kuwasogezea huduma za maji safi na salama karibu na makazi yao katika Jimbo la Mwibara?

Supplementary Question 1

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nina swali moja la nyongeza. Kwa kuwa kumtua mama ndoo kichwani mradi mkubwa ambao utasababisha hili litokee ni mradi wa Miji 26 ambao unafadhiliwa na Serikali ya India. Tunaomba kuuliza Mheshimiwa Waziri.

Ni lini mradi huu utaanza na umefikia wapi? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge lakini kama unavyotambua program ya kumtua mwana mama ndoo kichwani ni programu ya Mheshimiwa Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan. Serikali inatekeleza miradi mbalimbali ya maji kupitia bajeti ya Serikali lakini kupitia wadau mbalimbali wa maendeleo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kupitia Serikali ya India tunatarajia kutekeleza miradi ya Miji 28 zaidi ya dola milioni 500 na mpaka sasa hatua ambayo tumefikia taratibu zote za kimanunuzi kama Wizara ya Maji tumeshazikamilisha. Tunasubiri kibali (no objection) kutoka Exim Bank na hivi karibuni tutapata, katika kuhakikisha tunatekeleza miradi hiyo na wananchi waendelee kupata huduma ya maji safi na salama.

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA K.n.y. MHE. CHARLES M. KAJEGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza dhamira yake ya kuwatua Wanawake ndoo kichwani kwa kuwasogezea huduma za maji safi na salama karibu na makazi yao katika Jimbo la Mwibara?

Supplementary Question 2

MHE. SAMWEL X. HHAYUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Changamoto ya maji inayoikumba Jimbo la Mwibara ni sawasawa na ambayo tunaipata kwenye Mkoa wetu wa Manyara na sehemu kubwa huwa tunapata changamoto kubwa hasa kwenye eneo la kuchelewa kwenye suala la manunuzi. Pale Mkoani hatuna Afisa Manunuzi.

Je, Wizara iko tayari kwa kushirikiana na Utumishi kupeleka Afisa Manunuzi pale Mkoani ili kuharakisha manunuzi? Ahsante.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge wa Hanang kwa kazi kubwa na nzuri anayoifanya katika Jimbo lake. Sisi kama Wizara ya Maji tutaendelea kumpa ushirikiano katika kuhakikisha tunatatua matatizo ya maji katika Mkoa wa Manyara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala hili la Maafisa Manunuzi ni kweli tumeanzisha Taasisi yetu ya (RUWASA) Wakala wa
Maji Vijijini, hii ni mahususi kwa ajili ya kutatua matatizo ya maji vijijini. Lakini tumekuwa na changamoto ya watumishi hususani katika eneo la manunuzi. Tumeshafanya mazungumzo na wenzetu wa Utumishi na hivi karibuni tutapata Maafisa hao katika kuhakikisha tunakwenda kutatua matatizo ya maji. Eneo ambalo tutalipa kipaumbele kabisa ni Mkoa wa Manyara katika kuhakikisha hii changamoto tunaifanikisha kwa haraka. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA K.n.y. MHE. CHARLES M. KAJEGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza dhamira yake ya kuwatua Wanawake ndoo kichwani kwa kuwasogezea huduma za maji safi na salama karibu na makazi yao katika Jimbo la Mwibara?

Supplementary Question 3

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Kwa moyo wa dhati kabisa nimpongeze Mheshimiwa Aweso, kwetu sisi amejitahidi kuutendea haki Mradi wa Bunda umepiga hatua. Sasa ningependa kuuliza swali la nyongeza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Maji yametoka Nyabehu yamekuja Bunda Mjini. Katika mkataba wa ule mradi ilikuwa ni pamoja na kujengwa vituo. Hivi tunavyozungumza bado vituo havijajengwa Kata tu ya Gutagushigwamara hakuna kituo. Nyabeu yenyewe kiko kimoja, ukienda Kinyambwiga hakuna kituo, ukija Bunda Store huku hakuna kituo. Manyamanyama, Nyasura, Sazila hayo maeneo yote kama kungejengwa vituo tungeweza kupata maji katika Kata zote 14 kwa huo mradi uliochukua zaidi ya miaka 13. (Makofi)

Sasa kwa mujibu wa ule mkataba ni lini sasa hivyo vituo vitakamilika ili wananchi wa Halmashauri ya Mji wa Bunda Mjini wasahau biashara ya kupata shida ya maji safi na salama? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kazi kubwa na nzuri anayoifanya. Lakini nataka nimuhakikishie sisi kama Wizara ya Maji tumefanya mageuzi makubwa sana, kupitia Wizara yetu ya Maji na Rais wetu support kubwa ambayo anatupa ya kifedha. Tulikuwa na miradi kichefuchefu zaidi ya 177 asilimia nyingi tumekwisha ikamua. Sasa nataka nimpe mwaliko mahususi kabisa tarehe 7 Mheshimiwa Rais wetu mpenzi Mama Samia Suluhu Hassan atakuwepo Bunda. Naomba tujumuike ukaone kazi kubwa na nzuri ambayo imefanywa na Wizara yetu ya Maji katika Jimbo lako. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Assa Nelson Makanika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kaskazini

Primary Question

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA K.n.y. MHE. CHARLES M. KAJEGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza dhamira yake ya kuwatua Wanawake ndoo kichwani kwa kuwasogezea huduma za maji safi na salama karibu na makazi yao katika Jimbo la Mwibara?

Supplementary Question 4

MHE. ASSA N. MAKANIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza. Matatizo yaliyoko katika Jimbo la Mwibara na maeneo mengine ya Tanzania, yanafanana kabisa na matatizo yanayopatikana katika Jimbo la Kigoma Kaskazini. Ndani ya Jimbo la Kigoma Kaskazini tuna mradi wa Mkongoro I, ambao umechukua muda mrefu na huu mradi unakwamisha adhima ya Mheshimiwa Rais ya kumtua ndoo mama kichwani.

Naomba kujua ni lini huu mradi utaukamilisha ili tuweze kuwasaidia mama zetu katika Jimbo la Kigoma Kaskazini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge na nimeshafika katika Jimbo lake kiukweli unafanya kazi kubwa, unafanya kazi nzuri kama kijana. Sisi kama Wizara ya Maji tutaendelea kukupa ushirikiano. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi Wizara yetu ya Maji tumesema miradi ambayo imetumia kwa muda mrefu mkakati wetu ni kuhakikisha tunaikamilisha. Nikuombe Mheshimiwa Mbunge baada ya Bunge saa 7.00 tukutane tuone namna gani ya ku-push mradi ule ili tuweze kuukamilisha. Ahsante sana. (Makofi)