Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO K.n.y. MHE. GHATI Z. CHOMETE Aliuliza: - Je, ni lini agizo la Mheshimiwa Rais la kuboresha stendi ya Bweri Musoma Mjini litatekelezwa?

Supplementary Question 1

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, nina maswali mawili ya nyongeza. Kwa mujibu wa muuliza swali alitaka kujua ni lini Mheshimiwa Waziri hajajibu. Sasa na naendelea kuuliza ni lindi stendi hiyo itaboreshwa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, tatito lililopo katika stendi hiyo ya Bweri Musoma ni sawa kabisa na tatizo ambalo lipo katika stendi ya Mkoa katika Jimbo la Mtwara Mjini, stendi ipo eneo linaitwa Mkanaleli. Stendi ile ni mbaya sasa hivi mvua zinaponyesha maji yanatuama.

Je, nini mkakati wa Serikali kuhakikisha inaboresha stendi ile iendane na viwango kama zilivyo stendi katika mikoa mingine na majimbo mengine?

Mheshimiwa Mwenyekti, nakushukuru.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika majibu yangu ya msingi nimesema kwamba Serikali tayari imeanza mazungumzo na Benki ya BADEA ili kupata ufadhili kwa ajili ya kuanza ujenzi wa stendi ya Bweri katika Manispaa ya Musoma Mjini, na ujenzi huo utaanza wakati wowote mara fedha hizo zitakapopatikana.

Kwa hiyo, naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge wakati wowote fedha hizo zikipatikana kazi ya ujenzi wa stendi ile utaanza mara moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pili, kuhusiana na stendi ya Mkanaleli naomba nimpe wito Mheshimiwa Mbunge lakini pia niwaelekeze Mamlaka za Serikali za Mitaa kwamba, miundombinu hii yote stendi lakini na miundombinu mingine ipo chini ya Mamlaka za Serikali za Mitaa, wanawajibika kuhakikisha wanatenga bajeti kujenga au kukarabati stendi hizo lakini kama uwezo wa kibajeti hautoshelezi kutenga bajeti hizo basi wanaelekezwa kuandaa maandiko maalum kwa maana ya maandiko ya kimkakati ili kuweza kupata fedha kwa ajili ya ujenzi wa stendi hizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nitoe wito kwa halmashauri hiyo kuhakikisha wanafanya tathmini mara moja ya uhitaji wa ujenzi wa stendi hiyo na kuona uwezo wao wa kuijenga lakini kuomba miradi ya kimkakati ili Serikali iweze kusaidia kujenga stendi hizo. Ahsante.