Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 1 2022-02-02

Name

Ghati Zephania Chomete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO K.n.y. MHE. GHATI Z. CHOMETE Aliuliza: -

Je, ni lini agizo la Mheshimiwa Rais la kuboresha stendi ya Bweri Musoma Mjini litatekelezwa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) Alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla ya kujibu swali kwa ridhaa yako naomba nichukue fursa hii kwanza kumshukuru Mwenyezi Mungu Mwingi wa Baraka kwa kutujaalia afya njema sisi sote na kutuwezesha kuendelea na majukumu haya ya kuwatumikia watanzania wenzetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, nitumie fursa hii kumshukuru sana Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa imani kubwa aliyonipa na kuteua kuendelea kuwatumikia watanzania wenzetu katika dhamanahii muhimu ya Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, TAMISEMI. Naomba kumuahidi Mheshimiwa Rais kwamba nitafanya kazi kwa bidii yangu yote ili kuhakikisha imani yake na maono wake ya kuwatimizia maendeleo watanzania yanatimia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya maelezo ya utangulizi, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ghati Zephania Chomete, Mbunge wa Viti Maalum kama ifutavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, stendi ya mabasi ya Bweri katika Manispaa ya Musoma ilijengwa mwaka 2007 kwa mapato ya ndani ya halmashari kwa kutumia Mkandarasi CMG Construction Company Ltd aliyeingia mkataba wa shilingi bilioni 1.36 ambapo Mkandarasi huyo alifanya kazi zenye thamani ya shilingi milioni 921.17.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa stendi hiyo yenye uwezo wa kuingiza magari 35 hadi 45 ina miundombinu iliyochakaa hivyo inahitaji kuboreshwa. Kwa kutambua umuhimu wa stendi hiyo, tayari Halmashauri ya Manispaa ya Musoma imeandaa andiko la mradi huo na limewasilishwa Wizara ya Fedha na Mipango kwa ajili ya Uchambuzi wa kutengewa fedha kwa ajili ya ujenzi kupitia ufadhili wa Benki ya BADEA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea na utaratibu wa kupata ufadhili huo ili mradi huo pamoja na miradi mingine inayotarajiwa kutekelezwa kupitia ufadhili huo utekelezaji wake uweze kuanza. Ahsante.