Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafikisha umeme katika Kata za Nyanzwa, Udekwa na Ukwega Wilayani Kilolo?

Supplementary Question 1

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Nakiri ni kweli nimeona kazi hiyo inaendelea katika kata hizo zilizotajwa. Pamoja na hayo nina maswali yangu mawili madogo ya nyongeza: -

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza; katika utekelezaji wa miradi hii maeneo mengi ya huduma za jamii, hasa shule za msingi, shule za sekondari, makanisa na misikiti, hasa maeneo ambayo yako mbali kidogo na katikati ya miji, haziwekewi kipaumbele sana kupata umeme. Je, Serikali haioni kwamba ni vizuri kutenga bajeti maalum kwa ajili ya huduma za jamii, hasa sehemu ambazo watoto wetu wanasoma kwa sababu ni muhimu sana kuwa na umeme?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; katika miji mbalimbali midogo kwa mfano Mji wa Ilula uliopo Kata ya Nyalumbu, lakini pia Mji Mdogo wa Boma la Ng’ombe pamoja na Mji Mdogo wa Kidabaga, kumekuwa na kero kubwa ya kukatika umeme mara kwa mara. Je, Serikali ina mpango gani wa kumaliza kero hii? Ahsante.

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Nyamoga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba kwenye utekelezaji wa Mradi wa REA III, Mzunguko wa Pili, tuliwaelekeza wakandarasi wanaopeleka umeme katika maeneo yetu pamoja na wale wanaoshirikiana nao, wenzetu wa TANESCO, kuhakikisha kwamba maeneo ya taasisi na miundombinu mingine kama elimu, afya na taasisi za dini yanakuwa ni maeneo ya kipaumbele. Kama alivyosema Mheshimiwa Nyamoga, ni kweli maeneo yale ambayo tayari umeme umeanza kwenda kwenye maeneo ya makao makuu ya vijiji tayari tunapeleka.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Nyamoga pamoja na Waheshimiwa Wabunge wengine kwamba kadri tunavyozidi kupeleka umeme kwenye maeneo ya pembeni kwa maana ya vitongoji, tutazidi pia kufika katika taasisi hizo na ni maelekezo ya Serikali kwamba umeme ufike katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Spika, jambo lingine la kufurahisha zaidi ni kwamba, sisi Wizara ya Nishati pia tumepewa kipande kidogo cha bajeti katika ile 1,300,000,000 za Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan zinazopeleka maeneo ya UVIKO tunaopambana nao na sisi katika miundombinu hiyo mipya ambayo inajengwa tumepatiwa pesa kiasi fulani ambapo tutaweza kuongeza kasi ya kupeleka umeme katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Spika, kwenye eneo la pili, ni kweli kwamba kumekuwa kuna makatizo ya umeme kwenye maeneo mbalimbali, lakini ni jambo ambalo lililopangwa kwa ajili ya kufanya marekebisho ya miundombinu. TANESCO katika mwaka huu wa fedha inazo bilioni karibu zaidi ya 200 kwa ajili ya marekebisho ya miundombinu ya umeme katika maeneo mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, niwaombe Waheshimiwa Wabunge waendelee kutuvumilia kidogo tukiwa katika hatua hizi na harakati za kuhakikisha tunaboresha miundombinu yetu. Na kwa Iringa tuna takribani bilioni moja na milioni 500 kwa ajili ya marekebisho ya miundombinu. Tutaendelea kuwahimiza wenzetu watoe taarifa sahihi na kwa wakati sahihi ili Waheshimiwa umeme unapokatika, basi wananchi waweze kufahamu nini kinaendelea. Nakushukuru.

Name

Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Primary Question

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafikisha umeme katika Kata za Nyanzwa, Udekwa na Ukwega Wilayani Kilolo?

Supplementary Question 2

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi hii. Naomba niulize swali dogo tu la nyongeza. Kuna Mkandarasi anaitwa Giza mlituletea kwenye majimbo yetu, na mlimpa siku za kuja kwa Wabunge, mpaka leo tunamtafuta; nini kauli ya Serikali? Ahsante sana.

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, ni kweli nimepata concerns za baadhi ya Waheshimiwa Wabunge kuhusiana na Mkandarasi huyu Giza na kama alivyowahi kusema Mheshimiwa Mbunge mmojawapo kwamba jina la mkandarasi halivutii, lakini ni mmoja wa wakandarasi ambao walipata kazi katika Mradi wa REA II, round two katika Mikoa ya Manyara na Mara.

Mheshimiwa Spika, Waheshimiwa wamekuwa wakiniuliza mara kwa mara. Nitoe taarifa kwamba, tumemtafuta na tumempa maelekezo mahususi, nikitoka hapa nitawaeleza Waheshimiwa Wabunge ni namna gani tumechukua hatua ili aweze kufanya kazi yake na kuimaliza, ili inapofika hiyo Desemba 2022 ambayo tumekubaliana naye, tusiwe nje ya muda huo.

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafikisha umeme katika Kata za Nyanzwa, Udekwa na Ukwega Wilayani Kilolo?

Supplementary Question 3

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa nafasi hii ili niulize swali dogo tu la nyongeza. Ni lini sasa mkandarasi ambaye majuzi tu

Mheshimiwa Naibu Waziri alituambia hapa katika Bunge lako Tukufu kwamba anaanza kazi katika Halmashauri za Wilaya za Manyoni na Itigi ataanza kazi?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Yahaya kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuliwaelekeza wakandarasi wa lot hizo nne ambazo zilikuwa zimebakia, waripoti katika vituo vyao vya kazi wiki hii inayokwisha leo na ilikuwa ni kwenda kuangalia maeneo ya kupata go down za kutunza vifaa vyao na kuwasiliana na Waheshimiwa Wabunge.

Mheshimiwa Spika, kama Mheshimiwa Mbunge hajawasiliana na mkandarasi wake, naomba nitakapotoka hapa mimi mwenyewe nimuunganishe naye. Wiki inayokuja tunatarajia waanze kwenda kwenye maeneo hayo kwa ajili ya survey na kuanza kazi ambazo wameshasaini mikataba tayari. Nashukuru.