Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 9 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 94 2021-11-12

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itafikisha umeme katika Kata za Nyanzwa, Udekwa na Ukwega Wilayani Kilolo?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Lazaro Justin Nyamoga, Mbunge wa Kilolo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Kilolo ina kata 21, kati yake kata tatu tu hazijapata umeme na vijiji 94, kati yake vijiji 23 tu havijapata umeme. Vijiji vyote 23 ambavyo havina umeme vikiwemo Vijiji vya Kata za Nyanzwa, Udekwa na Ukwega ambavyo ni Nyanzwa, Mgowelo, Igunda, Udekwa, Wotalisoli, Ifuwa, Ukwega, Ipalamwa, Makungu na Mkalanga vinapatiwa umeme kupitia Mradi wa REA Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili ambao utekelezaji wake ulianza mwezi Machi, 2021 na unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba, 2022.