Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa kipaumbele wa kuongeza mtandao wa barabara za lami za Mji Mkongwe na wakitalii wa Mbamba Bay?

Supplementary Question 1

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza nianze kuishukuru sana Serikali kwa jitihada kubwa ambazo zimeshaanza katika kuboresha Mji huu wa Mbamba Bay. Lakini pamoja na shukrani hizo, ninapenda kupata majibu kutoka Serikalini, Mji huu wa Mbamba Bay ni mji ambao ni wa muda mrefu sana takribani miaka mia moja, lakini vilevile ni kitovu cha utalii katika Mkoa wa Ruvuma, lakini hiki kiasi cha kilometa moja, moja na nusu kinachotengwa ni kidogo kulinganisha na mahitaji yaliyopo kwa sababu mji huu umedumaa kwa muda mrefu.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba katika bajeti inayofuata angalau tupate hata kilometa mbili ili kuendana na kasi ya kukuza utalii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; Jimbo la Nyasa ni kubwa sana kwa ukubwa wake na jiografia milima mikali kiasi kwamba hawa TARURA ambao wanasimamia hizi barabara wanapata shida sana katika usimamizi kutokana na kuwa na gari bovu ambalo kila wakati linaendea matengenezo kutokana na hali halisi ya mazingira.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza gari jipya moja angalau kuwawezesha hawa watumishi wa TARURA waweze kutekeleza majukumu yao ipasavyo. (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Engineer Stella Martin Manyanya Mbunge wa Jimbo la Nyasa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli Mji wa Mbamba Bay ni Mji mkongwe na Mheshimiwa Mbunge kama alivyozungumza nafahamu jitihada kubwa ambazo anazifanya katika Jimbo lake na anahitaji tuongeze bajeti kuhakikisha ule mji unaongezewa lami.

Mheshimiwa Spika, kama tulivyoeleza katika swali letu la msingi kwamba tutaendelea kutenga fedha na katika mwaka wa fedha unaokuja kwa maana ya 2022/2023 basi Mji wa Mbamba Bay tutauongezea bajeti kwa ajili ya ujenzi wa kilometa walau moja ya lami nyingine ili kuongeza mtandao wa lami katika eneo hilo.

Mheshimiwa Spika, lakini suala la pili ameeleza kwamba Halmashauri ya Nyasa gari lake watu wa TARURA ni bovu na wanashindwa kufika katika maeneo korofi ni muhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Ofisi ya Rais, TAMISEMI kupitia Wakala wa Barabara Vijijini na Mjini tumeshaagiza magari mia moja ambayo tutayagawa katika Halmashauri za Wilaya 100 nchini ikiwemo Halmashauri ya Nyasa.

Kwa hiyo, hilo tunauhakika nalo atapata gari jipy. Ahsante. (Makofi)