Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 8 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 80 2021-11-11

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa kipaumbele wa kuongeza mtandao wa barabara za lami za Mji Mkongwe na wakitalii wa Mbamba Bay?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Engineer Stella Martin Manyanya Mbunge wa Jimbo la Nyasa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wakala wa Barabara Vijijini na Mjini (TARURA) inaendelea na ujenzi wa lami kilometa moja unaogharimu jumla ya shilingi milioni 473.50 unaotekelezwa na Mkandarasi VAG Contractors Ltd. katika eneo la Makao Makuu ya Wilaya kwa maana ya Bomani kwa mwaka wa fedha 2021/2022 pamoja na ujenzi wa kilometa 0.5 Kata ya Kilosa katika Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa.

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa eneo la Mbamba Bay kama eneo la utalii na shughuli za Uvuvi. Hivyo, Serikali itaendelea kutenga fedha kujenga barabara kwa kiwango cha lami kulingana na upatikanaji wa fedha katika eneo la Mbamba Bay.