Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Primary Question

MHE. STANSLAUS H. NYONGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya Kolandoto hadi Meatu?

Supplementary Question 1

MHE. STANSLAUS H. NYONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani na wewe mwenyewe ni shahidi, usanifu umefanyika toka mwaka 2017 mpaka leo tunakwenda miaka mitano, sita bado Serikali inatafuta fedha ya kujenga barabara hii kwa kiwango cha lami. Hivi kweli Serikali mko serious na ujenzi wa barabara hii? Mheshimiwa Flatei alitaka mpaka kupanda juu ya meza, hivi mnawaambia nini wananchi wa maeneo haya, Serikali mna mpango wa kujenga barabara hii lini? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili Mheshimiwa Waziri wananchi wa Maswa Mjini wanahitaji taa za barabarani kwa mujibu wa maelekezo yako Mheshimiwa Naibu Waziri taa 60 mmetuwekea taa 18 tu mwaka jana, mna mpango gani wa kumalizia taa zilizobaki katika mji wa Maswa? Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Stanslaus Haroon Nyongo Mbunge wa Maswa Mashariki kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge Serikali iko serious kuijenga barabara hii ambayo nimeitaja inayoanzia Lalago, Mwanuzi, Hydom, Mbulu hadi Karatu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na ninaomba nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika eneo la Mwanuzi-Sibiti kwenye bajeti hii tumetenga kuanza na ujenzi na zimetengwa billion 5 na tumetoa kibali lianze kwanza kujengwa daraja linaloitwa Itembe. Lakini katika barabara hiyo ambayo ni muendelezo kipande cha Mbulu Hydom tayari tumeshatangaza barabara kilomita 23 na tunaomba kipande chote kile kitangazwe, kwa hiyo muda wowote tutatangaza kilomita zote 50 ikiwa ni muendelezo wa hiyo barabara kuhakikisha kwamba yote inakamilika. Kwa hiyo, Serikali iko serious na ndio maana kazi zinaendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili naomba nimuhakikishie kwamba tuliahidi tutakamilisha hizo taa 60 na nitoe wito ama nitoe maagizo kwa Meneja wa Mkoa wa Simiyu kuhakikisha kwamba zoezi hili linakamilika kama tulivyoahidi kama Serikali, ahsante. (Makofi)

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. STANSLAUS H. NYONGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya Kolandoto hadi Meatu?

Supplementary Question 2

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Serikali imewekeza Bandari ya Kabo kwenye Wilaya ya Nkansi lakini changamoto kubwa ambayo inawafanya watu wasitumie bandari ile ni kwa sababu ya kukosa barabara ya kiwango cha lami cha kutoka Lyazumbi mpaka Kabwe na hiyo ni ahadi ya Mheshimiwa Waziri Mkuu. Ningependa kujua ni lini mtajenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Aida Khenani Mbunge wa Nkasi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Serikali imewekeza kujenga Bandari kubwa ya Kabwe ili tuweze kufungua Mkoa wa Rukwa na Tanzania kwa ujumla kufanya biashara na DRC Congo, na ndio maana tumejenga bandari mpya kabisa ya Kabwe. Lakini baada ya kujenga tunajua lazima kuwe na barabara, nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kazi ya kwanza barabara ilikuwa ni finyu.

Mheshimiwa Mweyekiti, kwa hiyo kazi ya kwanza ni kuipanua ile barabara madaraja tunayabadilisha yote na barabara tunaipanua na magari yote yaweze kupitika. Na baada ya hapo sasa mpango unaofuata ni kuijenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami lakini awamu ya kwanza ni kuipanua kubadilisha madaraja ili magari makubwa yaweze kupita.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Barabara ya Aliyazumbi Kabwe kama alivyoahidiwa na Mheshimiwa Waziri Mkuu itajengwa kwa kiwango cha lami, ahsante.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. STANSLAUS H. NYONGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya Kolandoto hadi Meatu?

Supplementary Question 3

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Serikali imetangaza kilometa 25 nashukuru. Je, bajeti ya sasa ina kilometa 50 ni lini sasa utatangaza kilometa 50 ili kufikia Hospitali ya Hydom barabara ile kujengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Flatei Massay Mbunge wa Mbulu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimhakikishie kwamba kipande cha kilomita 50 kati ya Hydom na Mbulu tumetangaza kilomita 25 na Wizara tayari imepeleka maombi maalum ili kipande chote kile kiweze kutangazwa na loti nzima ikamilike kwa hiyo tuko kenye hatua nzuri, ahsante.

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. STANSLAUS H. NYONGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya Kolandoto hadi Meatu?

Supplementary Question 4

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru sana kwa kunipa nafasi na mimi kuuliza swali la nyongeza. Kuna wakati fulani sisi wakazi wa Mikoa ya Kusini hasa Mtwara huwa tunafikiri kama huwa hatuonekani na Wizara hii ya Ujenzi, na ninasema hivyo kwa sababu kuna barabara inayotoka Mtwara, Nivata, Newala, Masasi ikipitia Kata za Chikunja, Lukuledi kuelekea Ndomoni Nachingwea mpaka Liweke ilitengewa kipande hichi cha Masasi Nachingwea kilitengewa kiasi cha shilingi billioni 1.5 tu, na tulimuuliza Waziri kwamba anategemea kuanza wapi katika hili alijibu lakini hakuwa wazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ninataka kufahamu kipindi cha mvua kinakaribia kuanza sasa hivi na baadhi ya maeneo mvua zimeanza kunyesha na barabara hii wakati wa mvua huwa ni usumbufu mkubwa huwezi kufika Newala kirahisi hauwezi kufika Nachingwea kirahisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa Serikali ilitenga shilingi billioni 1.5 sasa sisi tunataka kufahamu ni lini hasa na Serikali ituambie kinaga ubaga barabara hii inakwenda kutengenezwa na kukamilika sio maneno maneno yanayotokea sasa hivi. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cecil Mwambe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niwahakikishie Wabunge wa Mtwara, Newala, Masasi na Ndanda kwamba barabara hii ya kilomita 210 ya kuanzia Mtwara Nivata, Ndanda, Newala hadi Masasi tumeshajenga kilomita 50 bado kilomita 160. Naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tuko kwenye asilimia zaidi 85 na Benki ya Maendeleo ya Afrika iko tayari kuijenga hii barabara na tunauhakika kufikia mwishoni mwa mwezi wa 11 huu tutakuwa tumekamilisha mazungumzo na tunauhakika kwamba wako tayari kuijenga hii barabara. Na kipande hiki cha Masasi kwenda Nachingwea tayari tumeshatenga billion 1.5 kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge Serikali ya Awamu ya Sita haibabaishi ipo serious na kazi hii itafanyika ahsante. (Makofi)

Name

Ussi Salum Pondeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chumbuni

Primary Question

MHE. STANSLAUS H. NYONGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya Kolandoto hadi Meatu?

Supplementary Question 5

MHE. USSI SALUM PONDEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti ahsante sana, naomba nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri wa Ujenzi swali la nyongeza. Ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya lami katika Barabara ya Iboni, Bolisa na Gubali katika Jimbo la Kondoa Mjini? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ussi Pondeza Mbunge wa Chumbuni kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa barabara zile ambazo ziko Kondoa mjini barabara nyingi zinahudumiwa na halmashauri kwa zile barabara ambazo zinahudumiwa na Wakala wa Barabara TANROADS naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutajenga kama zilivyoainishwa kwenye mpango na kama ilivyo kwenye bajeti yetu ambavyo tumepanga, ahsante. (Makofi)