Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 7 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 76 2021-11-10

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Primary Question

MHE. STANSLAUS H. NYONGO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya Kolandoto hadi Meatu?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi ninapenda kujibu Swali la Mheshimiwa Stanslaus Haroon Nyongo, Mbunge wa Maswa Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Barabara ya Kolandoto – Mwanhuzi (Meatu) yenye urefu wa kilometa 117.57 ni sehemu ya Mradi wa Barabara ya Kolandoto – Lalago – Mwanhuzi – Sibiti – Oldeani B Junction yenye urefu wa kilometa 328 usanifu wake ulikamilika mwaka 2017. Serikali inaendelea na jitihada na juhudi za kutafuta fedha ili kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati Serikali ikiendelea na juhudi za kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami, Wizara yangu kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) inaendelea kuifanyia matengenezo mbalimbali barabara hii ili iendelee kupitika majira yote ya mwaka. Katika mwaka wa fedha 2021/2022 jumla ya shilingi milioni 1,240.246 zimetengwa kwa ajili ya kazi hiyo, ahsante. (Makofi)