Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kilumbe Shabani Ng'enda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Mjini

Primary Question

MHE. KILUMBE S. NG’ENDA aliuliza: - (a) Je, nini matokeo ya Utafiti wa mafuta uliofanyika katika Ziwa Tanganyika zaidi ya miaka mitatu iliyopita? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuvuna mafuta hayo?

Supplementary Question 1

MHE. KILUMBE S. NG’ENDA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza. Kwa kuzingatia taarifa iliyotolewa na Serikali ni kwamba kampuni iliyokuwa inafanya utafiti ya Beach Petroleum tangu mwaka 2017 imeshindwa kuendelea na kazi hiyo kutokana na kina kirefu cha maji na wenyewe kushindwa gharama hiyo: -

Je, Serikali imetafuta mwekezaji mwingine katika eneo hilo tokea hiyo 2017? Kama hivyo ndiyo, wananchi wategemee lini utafiti huo kukamilika?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kilumbe Ng’enda, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tangu mwaka 2017 pale ambapo kitalu kilirudishwa na mwenzetu wa beach petroleum mtakumbuka kwamba kulikuwa kuna upiatiaji wa mikataba ya uvunaji na ushirikiswaji (PSA) na hivyo tangu kipindi hicho Serikali haijatangaza vitalu wazi kwa ajili ya wawekezaji kuja kufanya utafiti katika maeneo hayo. Hivyo, baada ya PSA Review kuwa zimekamilika sasa Serikali iko tayari kuanza kutanganza ili watu sasa waweze kuja kuwekeza katika maeneo hayo kwa ajili ya kufanya utafiti na baadaye kubaini uwepo wa mafuta na kuanza kuyatumia.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Kilumbe Ng’enga kwamba Serikali iko katika hatua za kuhakikisha inakamilisha hiyo taarifa ya PSA Review na baada ya kufanya reviews zikakamilika, itaweza kufungua kwa ajili ya kuweza kukaribisha sasa watu kuja kuendelea na utafiti. Itakapofanya hivyo, basi taarifa ya nini kimepataikana itatolewa. Nakushukuru.

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KILUMBE S. NG’ENDA aliuliza: - (a) Je, nini matokeo ya Utafiti wa mafuta uliofanyika katika Ziwa Tanganyika zaidi ya miaka mitatu iliyopita? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuvuna mafuta hayo?

Supplementary Question 2

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Utafiti kama huo ambao umefanyika Ziwa Tanganyika umewahi kufanyika pia katika Ziwa Eyasi katika Jimbo la Karatu kuhusu upatikanaji wa mafuta katika ziwa hilo. Je, utafiti huo umekamilika au bado na je, matumaini ya kupata mafuta yapo?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cecilia Paresso, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tunalo bonde linaitwa Bonde la Eyasi Wembere ambalo linatoka Singida, linapita Tabora, linapita Simiyu na kipande cha Manyara pia kipo. Utafiti katika bonde hilo unafanywa na Shirika letu la TPDC na kwenye Bonde la Eyasi-Wembere bado tunaendelea na utafutaji wa awali wa kujua maeneo ambayo tunaweza tukapata mafuta au gesi katika maeneo hayo. kwa hiyo, utafutaji bado unaendelea na utakapokuwa umekamilika, basi utapata matunda ya kuweza kuvuna gesi na mafuta.