Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 6 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 68 2021-11-09

Name

Kilumbe Shabani Ng'enda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Mjini

Primary Question

MHE. KILUMBE S. NG’ENDA aliuliza: -

(a) Je, nini matokeo ya Utafiti wa mafuta uliofanyika katika Ziwa Tanganyika zaidi ya miaka mitatu iliyopita?

(b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuvuna mafuta hayo?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kilumbe Shabani Ng’enda, Mbunge wa Kigoma Mjini, lenye sehemu
(a) na (b) kwa pamoja kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, utafiti wa mafuta katika Ziwa Tanganyika umegawanywa katika vitalu viwili; Kaskazini na Kusini. Katika kipindi cha mwaka 2015/2016, TPDC ilikusanya taarifa za uvutano wa usumaku zenye jumla ya urefu wa kilomita 24,027 za mstari katika kitalu cha Ziwa Tanganyika Kaskazini. Tathmini ya taarifa hizo pamoja na taarifa za kijiolojia na kijiofizikia zilizopatikana katika eneo la mradi zimewezesha kugundua na kutenga maeneo yenye uwezekano wa kuwepo kwa mashapo ya kuhifadhi rasilimali (petroleum).

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Shirika la Maendeleo Nchini (TPDC) kwa kushirikiana na Mwekezaji kutoka Kampuni ya Beach Petroleum ilifanya utafiti wa mafuta katika kitalu cha Ziwa Tanganyika Kusini kuanzia mwaka 2010 mpaka mwaka 2017. Taarifa za utafiti huo ziliwezesha kubaini miamba yenye uwezekano wa kuhifadhi mafuta. Hata hivyo, changamoto za uchimbaji kisima katika Ziwa Tanganyika zilizomkabili Mwekezaji alishindwa kusafirisha vifaa vya kuchoronga kutokana na kina kirefu cha maji katika Ziwa Tanganyika na upatikanaji wa fedha zilisababisha Mwekezaji kushindwa kuendelea na utafiti na hivyo kulazimika kurudisha kitalu kwa Serikali mnamo mwaka 2017 kwa kuzingatia sheria zetu za mafuta na gesi.

Mheshimiwa Spika, pamoja na uwepo wa viashiria vizuri vya mafuta katika vitalu vya Ziwa Tanganyika, mpaka sasa Serikali haijagundua mafuta wala gesi katika eneo hilo. Katika mwaka wa fedha 2021/2022 TPDC inatarajia kuendelea kufanya tathmini ya kina ya takwimu za usumaku kwa Kitalu cha Ziwa Tanganyika Kaskazini. Takwimu hizi zitatumika kutengeneza mpango wa kukusanya takwimu za mitetemo kwa ajili ya kuainisha na kuhakiki uwepo wa mashapo ya kuhifadhi mafuta na gesi. Nakushukuru. (Makofi)