Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. VITA R. KAWAWA K.n.y. MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupelekea maji katika Vijiji vya Lingusenguse, Lusewa, Namwinyu, Mchomoro na Luchiri Wilayani Namtumbo?

Supplementary Question 1

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa, bado Mji wa Namtumbo una uhaba mkubwa wa maji na kwa kuwa kuna fedha hizi za UVIKO zinazohusiana na sekta ya maji, Serikali inaweza ikaelekeza fedha hizo RUWASA wakazielekeza katika ukarabati wa chanzo cha maji kinacholeta maji Namtumbo na kutandaza bomba la maji jipya? Kwa sababu, chanzo hicho ni cha toka mwaka 1980 ili kutatua tatizo la maji ya pale Namtumbo Mjini? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili kwa kuwa pia tuna miradi ya maji ya Luhimbalilo na Ikesi na maji ya Kumbala, Litola, miradi hii imekuwa kizungumkuti bado hatujui itaisha lini. Je, Serikali mnaweza mkaja mkatusaidia kuona nini kinachokwamisha ucheleweshaji wa miradi hii miwili? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Jacqueline Ngonyani yaliyoulizwa na Mheshimiwa Vita Kawawa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, fedha za UVIKO kutumika kwenye kuboresha chanzo cha maji. Hizi fedha za UVIKO sisi kama Wizara tumeelekeza kwenye miradi ambayo itakwenda kukamilika na kuleta huduma mara moja kwa jamii. Tunataka miradi ambayo inaleta majawabu kwa haraka hivyo, namna ambavyo Mkoa umeelekeza ile fedha ni sahihi. Kuhusiana na kazi hii ya kukifanyia hiki chanzo cha maji kinachotegemewa pale Namtumbo, tutatumia fedha za Mfuko wa Maji kuhakikisha kwamba tunakuja tunahakikisha chanzo kinatumika kikamilifu kwani vyanzo ni vichache. Hivyo, tunapopata vyanzo kama hiki tutakitumia kikamilifu ili kuleta tija kwenye jamii yote ya Namtumbo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na Vijiji vya Ikesi pamoja na hivyo vingine, Serikali inatoa jicho la kipekee kabisa kuona kwamba maeneo haya ambayo kwa muda mrefu yamepata shida ya maji, tunakuja kuleta ufumbuzi na maji bombani yatapatikana kwa wananchi. (Makofi)

Name

Philipo Augustino Mulugo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songwe

Primary Question

MHE. VITA R. KAWAWA K.n.y. MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupelekea maji katika Vijiji vya Lingusenguse, Lusewa, Namwinyu, Mchomoro na Luchiri Wilayani Namtumbo?

Supplementary Question 2

MHE. PHILLIPO A. MULUGO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Jimbo la Songwe ni pana ni kubwa na lina vijiji viko very scattered na kutoka kijiji kwenda kijiji baadhi ya vijiji kuna Mito kama Maleza au Rukwa na Some. Sasa, tuko Novemba sasa na tayari watu wa RUWASA wanatuambia tumeshapata fedha kwa ajili ya kupeleka maji kwenye vijiji hivyo. Lakini mpaka sasa hatujaona wakandarasi kuanza kazi sehemu hizo na sehemu nyingi Tanzania nzima watu wa RUWASA wanasema wanafanya manunuzi lakini wanachelewa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa Serikali naomba ituambie ni lini hasa Wakandarasi wataanza kumwagika kwenye Wilaya zetu kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maji? Ukizingatia tunaenda kwenye wakati wa mvua? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza kutoka kwa Mheshimiwa Phillipo Mulugo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wakala wa Maji na Usambazaji wa Maji Vijijini RUWASA ni kweli palikuwa na changamoto katika eneo la ununuzi lakini tayari Mheshimiwa Waziri amewaagiza na wamejipanga. Kipekee nimpongeze Engineer Kivigalo anafanya kazi nzuri ambaye ni DG wa RUWASA. Usimamizi wa kufanya manunuzi yaende kwa wakati sasa hivi utakuwa umeshaboreshwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lini tunakuja tayari tupo kazini sisi Wizara ya Maji, katika eneo lako huenda ndiyo limechelewa tu kupata wakandarasi lakini maeneo mengi kazi zinaendelea. Hivyo, nikutoe hofu Mheshimiwa Mbunge baada ya hapa tuonane tuone tunaweka sawa mambo kazi zikaanze mara moja. (Makofi)

Name

Kunti Yusuph Majala

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. VITA R. KAWAWA K.n.y. MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupelekea maji katika Vijiji vya Lingusenguse, Lusewa, Namwinyu, Mchomoro na Luchiri Wilayani Namtumbo?

Supplementary Question 3

MHE. KUNTI Y. MAJALA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi na mimi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Jiji la Dodoma takribani sasa ni miezi mitatu mfululizo kumekuwa na mgao wa maji usiokuwa na taarifa. Leo mitaa mbalimbali kwenye Kata ya Ipagala, Kata ya Dodoma Makulu, lakini Kata ya Nzuguni wana siku ya tano hakuna maji.

Nataka kupata kauli ya Serikali ina mkakati gani madhubuti wa dharura wa kuondoa changamoto hii kubwa inayowakumba wakazi wa Dodoma, lakini na wageni mbalimbali wanaoingia kwenye Jiji letu hili kufanya shughuli zao mbalimbali? Kwa sababu, imekuwa ni kero kubwa sana.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kunti, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli Jiji la Dodoma tumepitia kidogo changamoto katika mitambo yetu ya Mzakwe na pale Mailimbili. Tatizo kubwa ilikuwa ni umeme na tumewasiliana kwa karibu sana Mheshimiwa Waziri Aweso, pamoja na Mheshimiwa Makamba. Wamefanyia kazi hili suala kwa pamoja kuona kwamba lane ile ya umeme inayofanya uwezeshaji pale kwenye vile vyanzo usiwe disturbed. Kwa sababu, imekuwa disturbed huko mbele kulingana na ugawaji huu wa umeme wa REA, lakini sasa hivi wanaendelea kufanya maboresho ili kuona kwamba umeme usikatike kwenye vyanzo vyetu.

Mheshimiwa Spika, kwa dharura sana pale inapobidi sana Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira hapa Dodoma anajitahidi kuona kwamba maboza yanazunguka huko kutoa huduma pale inapobidi sana, lakini tayari maji yanarejea katika mfumo wake baada ya umeme kidogo kuwa unapatikana.

SPIKA: Labda Mheshimiwa Waziri kwa kuunganisha tu. Kwa kuwa ufumbuzi wa uhakika ni maji haya kutoka Ziwa Victoria, nini kinaendelea hivi sasa kutoka Ziwa Victoria kuja Mji wa Dodoma? (Makofi)

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, mradi wa maji kutoka Ziwa Victoria kuja hapa Dodoma ni katika miradi yetu mikubwa ambayo tunategemea fedha kutoka nje. Wiki iliyoisha siku ya Ijumaa Wizara (wataalam) waliweza kuketi na World Bank kuendelea kufanya mazungumzo kuona huu mradi sasa unaingia kwenye utekelezaji.