Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 6 Water and Irrigation Wizara ya Maji 63 2021-11-09

Name

Jacqueline Kandidus Ngonyani (Msongozi)

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. VITA R. KAWAWA K.n.y. MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kupelekea maji katika Vijiji vya Lingusenguse, Lusewa, Namwinyu, Mchomoro na Luchiri Wilayani Namtumbo?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jacqueline Ngonyani Msongozi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nia ya Serikali ni kuhakikisha huduma ya upatikanaji wa maji inaboreshwa katika Wilaya ya Namtumbo, ambapo kwa sasa hali ya upatikanaji wa huduma ya maji Wilayani humo ni asilimia 69. Katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali inaendelea kuboresha huduma ya maji katika Halmashauri hiyo ambapo katika Vijiji vya Lingusenguse, Lusewa na Mchomoro kazi zinazoendelea ni pamoja na ukarabati wa pampu ya mkono, ujenzi wa chanzo, ukarabati wa tanki la ujazo wa lita 50,000, ujenzi wa vituo vya kuchotea maji (16) na ulazaji wa bomba la kusambaza maji urefu wa kilomita tisa. Kazi zote zinatarajiwa kukamilika mwezi Januari, 2022.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa Kijiji cha Namwinyu ujenzi wa mradi utaanza robo ya tatu ya mwaka 2021/2022 na utahusisha uchimbaji wa kisima kirefu, vituo vinne (4) vya kuchotea maji, ulazaji wa bomba kilomita tatu (3) na ujenzi wa tanki la kuhifadhia maji la lita 90,000.

Mheshimiwa Spika, katika Kata ya Luchili wananchi wa Vijiji vya Namanguli, Misufini, Chengena na Kilangalanga wanapata huduma ya maji kupitia visima 24 vinavyotumia pampu za mkono. Katika mwaka 2021/2022, Serikali kupitia RUWASA itachimba visima virefu viwili (2) na kujenga miundombinu ya kusambaza maji. Kazi hizo zinatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2022.

Mheshimiwa Spika, kukamilika kwa utekelezaji wa miradi hiyo kutaondoa tatizo la maji katika vijiji vilivyotajwa. (Makofi)