Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwanaisha Ng'anzi Ulenge

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaruhusu usafirishaji wa Viumbe Hai nje ya nchi?

Supplementary Question 1

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza; kwa kuwa, miongoni mwa viumbe hai waliozuiliwa ni pamoja na vipepeo ambao sio maliasili, vipepeo wanaozalishwa na watu binafsi Wilayani Muheza, Mkoani Tanga. Je, Serikali iko tayari kutoa tamko rasmi kwamba, masharti waliyoyatoa yatawahusu viumbe hai ambao ni maliasili na vimbe hai wanaozalishwa na watu binafsi hayawahusu? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; Mto Zigi, Mkoani Tanga, una mamba wengi ambao wanaua watu wengi kwa muda mrefu sana. Tangu nikiwa binti mdogo watu wanafariki na juzi tu kuna mtu ameliwa na mamba na vilevile watu watatu wameshaliwa na mamba miezi miwili iliyopita. Je, Serikali haioni haja ya kwenda kuvuna mamba wale hata kama mto ule hauko ndani ya hifadhi, lakini mamba ni maliasili? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Engineer Mwanaisha Ulenge, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimshukuru sana Mheshimiwa Mwanaisha kwa maswali mazuri ambayo ameyaelekeza kwa Serikali, likiwemo hili la wanyamapori hai. Nataka nimwondoe wasiwasi, tunaposema wanyamapori hai ni wanyama wa aina yoyote iwe mdudu, nani, anaposafirishwa nje ya nchi sisi kama Maliasili na Utalii tunatambua kwamba, hiyo ni rasilimali ya nchi na haipaswi kuhamishwa kutoka eneo moja kwenda nje ya nchi. Kwa hiyo, nataka nimtoe wasiwasi na ndio maana hata hawa mamba pengine hawapo hata kwenye hifadhi, lakini kwa kuwa ni maliasili za Taifa lazima tuzilinde. Tunazilinda ili tuweze kuleta watalii ndani ya nchi waje kuona na tunapata mapato kutokana na vivutio hivi tulivyonavyo.

Mheshimiwa Spika, kwa kifupi maswali yote nimeyajibu kwa pamoja, lakini hili la kuvunwa mamba nimtoe wasiwasi, mwezi uliopita tulikuwa tuna tathmini ya kukusanya data ya mamba wote ambao wamekuwa wakisumbua wananchi. Tayari tuko kwenye mkakati wa kwenda kuwavuna, hivyo muda wowote ninavyosema kuanzia sasa, tutatuma wataalam wa kwenda kuvuna mamba hao. Naomba kuwasilisha.