Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 5 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 54 2021-11-08

Name

Mwanaisha Ng'anzi Ulenge

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaruhusu usafirishaji wa Viumbe Hai nje ya nchi?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Engineer Mwanaisha Ng’anzi Ulenge, Mbunge wa Viti Malum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tarehe 17 Machi, 2016 Serikali ilisitisha biashara ya kusafirisha wanyamapori hai nje ya nchi. Tatizo kubwa lililosababisha maamuzi hayo lilikuwa ni matokeo hasi yaliyokuwa yakiendelea kujitokeza kutokana na kufanya biashara hiyo ikiwemo kuhamisha rasilimali ya wanyamapori nje ya nchi. Aidha, Serikali ilirejesha jumla ya shilingi 173.2 ya ada na tozo zilizolipwa awali na wafanyabiashara kabla ya kusitishwa kwa biashara hiyo.

Mheshimiwa Spika, Serikali imefanya tathmini ya kina kuhusu biashara ya usafirishaji wa wanyamapori hai nje ya nchi. Kufuatia tathmini hiyo, zuio la biashara litaondolewa ambapo biashara hiyo itafanyika kwa utaratibu ufuatao: -

(i) Wanyamapori hai wataruhusiwa kusafirishwa kwa shughuli za utafiti na kidiplomasia tu.

(ii) Wanyamapori watakaosafirishwa nje ya nchi watakuwa ni wale waliokaushwa au mazao yatokanayo na wanyamapori hao.

(iii) Biashara ya wanyamapori waliokaushwa pamoja na mazao yake itafanywa na wafanyabiashara wenye miradi ya ufugaji wanyamapori ili kuhamasisha uanzishwaji wa miradi ya ufugaji wa wanyamapori.

(iv) Serikali itatoa muda wa miezi mitatu ili kuruhusu wafanyabiashara kusafirisha wanyamapori waliosalia kwenye mazizi na mashamba kabla ya zuio ambao walikuwa wanafugwa kwa lengo la kuwasafirisha nje ya nchi.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.