Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE.COSATO D. CHUMI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa GN kuwezesha Mradi wa Regrow kuanza rasmi katika eneo la Kihesa?

Supplementary Question 1

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Kwanza naishukuru Serikali kwa kuifanya Iringa kuwa kitovu cha utalii kusini, lakini mradi huu ambao GN hiyo imetangwazwa Julai, 2021 ulizinduliwa tarehe 12 Februari, 2018 na Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hassain akiwa Makamu wa Rais. Sasa swali langu ni moja tu kwa Serikali, je, inaridhika na speed ya utekelezaji wa mradi huu?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa David Chumi, Mbunge wa Mafinga Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge kwamba mradi huu utakamilika kwa wakati. Nasema hivyo kwa sababu mradi huu una-cover maeneo manne ya Kusini mwa Tanzania ambako ndiyo unatekelezwa. Mradi huu kwenye maeneo haya ni pamoja na Hifadhi ya Nyerere, Ruaha, Udzungwa na Mikumi.

Mheshimiwa Spika, eneo analoliongelea Mheshimiwa Chumi ni eneo mojawapo ambalo ni ujenzi wa kituo mahususi kwa ajili ya kutunza information za masuala ya utalii. Hivyo, maeneo mengine mradi huu unaendelea ambapo mitambo mbalimbali imeshanunuliwa, magari lakini pia kuna viwanja vya ndege ndani ya hifadhi vimeendelea kukarabatiwa na miundombinu mingine mingi inaendelea kufanyika. Hivyo, eneo hili lilikuwa linasubiri tu GN iweze kukamilika, lakini wakati huo huo tuna mshauri mwelekezi ambaye tayari ameshaanza zoezi na tumeshaanza kupokea ripoti. Kwa hiyo, nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge kwamba tutakamilisha mradi huu kwa wakati bila wasiwasi. Ahsante. (Makofi)