Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Daraja la Gunyoda ambalo linaunganisha Halmashauri ya Mji wa Mbulu, Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu na Halmashauri ya Wilaya ya Karatu hususani Tarafa ya Mang’ola kwenye mashamba ya vitunguu?

Supplementary Question 1

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali kupitia Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali langu la kwanza; nini kauli ya Serikali kwa kuwa Daraja la Gunyoda limepoteza maisha ya wakazi wa Jimbo la Mbulu Mji hasa nyakati za masika? Kwa kuwa daraja hilo ni kubwa na linaunganisha halmashauri mbili imekuwa kikazo kikubwa sana kwa huduma za kijamii.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kwa kuwa tatizo la kuongezeka kwa makorongo katika nchi yetu limekuwa kubwa na tatizo hili linachochewa na mabadiliko ya tabianchi. Je, Serikali haioni umuhimu sasa wa kutuma Watalaam wa Wizara, Mkoa na Halmashauri zote nchini ili wafanye mapitio upya katika maeneo haya ili waandae mpango wa kuzuia kuongezeka kwa makorongo, lakini pia na ujenzi wa maeneo ambayo yatapewa kipaumbele katika bajeti za Serikali?

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Zacharia Paulo Issaay, Mbunge wa Jimbo la Mbulu Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza anataka kauli ya Serikali juu ya hilo korongo ambalo linatakiwa kujengwa daraja. Nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge asiwe na wasiwasi Serikali ya Awamu ya Sita, moja ya kazi yake kubwa ambayo tumekubaliana kuifanya sasa hivi ni kuunganisha maeneo yote kwa kujenga madaraja hususani katika maeneo korofi. Kwa hiyo na daraja hili katika mpango wa fedha wa mwaka unaofuatia tutaliweka katika vipaumbele vyetu kuhakikisha daraja hili na lenyewe linapatiwa fedha ili liweze kujengwa kwa umuhimu ambao Mheshimiwa Mbunge ameusema hapa kwamba daraja hili linaunganisha halmashauri mbili kwa maana ya Mbulu Mji na Halmashauri ya Mbulu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, lilihusu maongezeko ya makorongo, akawa anataka Serikali tufanye tathimini upya kwa kutuma watalaam ili tuweze kuzuia uendelezaji huu. Moja; nipokee kama ushauri kwamba sisi kama Serikali tumepokea, lakini la pili; ni kwamba kwa hivi karibuni tulishawatuma wahandisi wetu nchi nzima kukagua na kuanisha maeneo yote korofi hususani madaraja ili tuweze kuyatengea bajeti na yaweze kupitishwa. Kwa hiyo na hili ni sehemu ya mapendekezo ambayo ameyatoa na sisi tunaendelea kuyapokea. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Daraja la Gunyoda ambalo linaunganisha Halmashauri ya Mji wa Mbulu, Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu na Halmashauri ya Wilaya ya Karatu hususani Tarafa ya Mang’ola kwenye mashamba ya vitunguu?

Supplementary Question 2

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa swali la msingi linazungumzia korongo lililopo katika Wilaya ya Mbulu Mji ambalo linaenda mpaka Wilaya ya Karatu na katika Tarafa ya Yasi ambako kuna wakulima wa vitunguu katika maeneo hayo. Sasa je, Serikali haioni ipo haja ya kuikutanisha TANROADS Mkoa wa Arusha kwa maana ya Wilaya ya Karatu na TANROADS Mkoa wa Manyara ili kwa pamoja kuwe na nguvu ya kuhakikisha haya madaraja ambayo yanaathiri wilaya mbili yanapatiwa ufumbuzi ili wananchi waweze kufanya shughuli zao kama inavyotakiwa.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Cecilia Paresso, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nikubali na nipokee ushauri wa Mheshimiwa Mbunge kwa sababu Serikali ni moja na tunafanya kazi kama wamoja, basi kwa kutumia hadhara hii niahidi tu kwamba tutakaa pamoja na watu wa ujenzi kuhakikisha, hao TANROADS Arusha na Manyara wanakutana na kufanya tathmini katika maeneo hayo ambayo Mheshimiwa Mbunge ameyaainisha. Kwa hiyo tumepokea ushauri wake na tutaufanyia kazi. Ahsante.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Daraja la Gunyoda ambalo linaunganisha Halmashauri ya Mji wa Mbulu, Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu na Halmashauri ya Wilaya ya Karatu hususani Tarafa ya Mang’ola kwenye mashamba ya vitunguu?

Supplementary Question 3

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo. Jimbo la Mji Korongo hili la Gunyoda linalosemwa lipo kwenye barabara moja hiyo hiyo kuja Jimbo la Mbulu Vijijini, lipo korongo la Hudaya ambalo lina thamani kubwa ya 1,200,000,000.

Je, Serikali ipo tayari sasa na hii ya Hudaya kuweka kwenye mpango kwa sababu ukiweka hili la Gonyoda la Hudaya utakuwa hujaweka kwenye mpango wa kujengwa barabara hiyo itakuwa haitumiki kabisa.
Je, Waziri yupo tayari na hili ili barabara itumike?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza Mheshimiwa Flatei Massay, Mbunge wa Mbulu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, niseme tu kwamba kwa sababu na hili ni ombi jipya na bahati nzuri lilishafanyiwa tathmini na gharama ya fedha na jukumu letu sisi kama Serikali ni kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa hayo madaraja. Kwa hiyo na lenyewe nilipokee tutaenda kushauriana na wataalam ili na lenyewe tuliingize katika mpango wa awamu inayofuatia. Ahsante. (Makofi)

Name

Kiswaga Boniventura Destery

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magu

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Daraja la Gunyoda ambalo linaunganisha Halmashauri ya Mji wa Mbulu, Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu na Halmashauri ya Wilaya ya Karatu hususani Tarafa ya Mang’ola kwenye mashamba ya vitunguu?

Supplementary Question 4

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Napenda kuuliza swali la nyongeza moja. Rais aliyepita, Mheshimiwa Magufuli alituahidi kutujengea daraja kutoka Kata ya Ifunda kwenda Kata ya Lumuli sasa napenda kujua, je, tumefikia hatua gani kutekeleza hiyo ahadi? Ahsante sana.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la dogo la nyongeza la Mheshimiwa Kiswaga, Mbunge wa Kalenga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie kwamba Serikali ya Awamu ya Sita, moja ya mpango wetu ni kwamba ahadi zote za Viongozi Wakuu na Viongozi wetu Wastaafu na ile ambayo ilitolewa na Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, zote zipo katika mipango ya utekelezaji wa Serikali. Kwa hiyo, aondoe shaka zipo pale na Serikali inachosuburi tu ni namna ya kuzitekeleza. Ahsante sana.