Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 3 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 31 2021-11-04

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Daraja la Gunyoda ambalo linaunganisha Halmashauri ya Mji wa Mbulu, Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu na Halmashauri ya Wilaya ya Karatu hususani Tarafa ya Mang’ola kwenye mashamba ya vitunguu?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zacharia Paulo Issaay, Mbunge wa Jimbo la Mbulu Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imekwishachukua hatua za kufanya upembuzi wa awali kwenye Korongo la Gunyoda lililoko katika Barabara ya Waama-Masieda, Kata ya Gunyoda katika Halmashauri ya Mji wa Mbulu ambako ndiko daraja hilo litajengwa. Korongo hilo lina urefu wa mita 70.4 na kina cha mita 5.0. Kutokana na ukubwa wa korongo hilo, upembuzi ulibainisha kuwa, ili kujenga Daraja la Gunyoda zinahitajika shilingi bilioni 1.2. Fedha hizi ni zaidi ya ukomo wa bajeti ya Halmashauri katika Fedha za Mfuko wa Barabara.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, kwa kuona umuhimu wa daraja la Gunyoda ikizingatiwa daraja hilo linaunganisha Halmashauri ya Mji wa Mbulu, Serikali inaendelea kutafuta fedha ili kuhakikisha daraja hilo linajengwa kulingana na upatikanaji wa fedha.