Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha Mradi wa Maji katika Vijiji vya Ikelu, Ibatu, Mtulingala, Nyamande, Usetule Mahongole Wilayani Makambako?

Supplementary Question 1

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Spika, naishukuru Serikali. Pamoja na majibu mazuri ya wananchi wa vijiji hivi ambavyo vimetajwa, nilikuwa na maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza: Pamoja na Naibu Waziri kutamka hapa kwamba vijiji hivi vitapata maji mwakani na kingine cha Ikelu kina asilimia 98: Tatizo ambalo lipo aniambie hapa, Wakandarasi hawa wamesimama, hawaendelei kwa sababu hawajalipwa fedha; ni lini watalipwa fedha ili waweze kukamilisha miradi hii? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili: nazungumza kwa uchungu, Pamoja na kwamba Wizara ya Maji wanafanya kazi nzuri sana na Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hassan, Rais wetu wa Awamu ya Sita, kazi yake ni nzuri sana. Kuna jambo ambalo nataka nizungumzie hapa unisaidie katika miji 28 ambayo ilikuwa ipate maji kupitia fedha za mkopo nafuu kutoka India, limezungumzwa kwa muda mrefu, mojawapo ni Makambako nayo ipo kwenye miradi hiyo… (Makofi)

SPIKA: Sasa swali Mheshimiwa.

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Spika, sasa swali. Katika Mji wa Makambako ambao unategemea mradi huu mkubwa, una Kata tisa. Unapitiwa na Kata tisa. Wananchi hawa tumekuwa tukiwaambia kwa muda mrefu: Ni lini Mkandarasi atakwenda kuanza kutengeneza mradi huu? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Deo Kasenyenda kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, naomba kusema Wakandarasi tayari malipo yanaendelea na malipo tunalipa kwa awamu kadri ambavyo tunapata fedha. Ninaamini hata Wakandarasi wa Makambako nao kwa mgao wa mwezi huu wa Kumi ambao tunaugawa mwezi huu wa Kumi na Moja, nao wataingizwa katika malipo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na miji 28, napenda kumshukuru Mheshimiwa Waziri wetu Mheshimiwa Jumaa Hamidu Aweso, amefatilia kwa karibu sana suala hili na tayari wakandarasi wapo; na wenzetu kutoka Benki ya Exim kutoka India wamefika Tanzania, hapa Dodoma juzi na jana pia tulikuwa na kikao nao. Hivi ninavyoongea kikao kinaendelea ndiyo maana Mheshimiwa Waziri hapa hayupo. Kwa hiyo, niseme tupo mwishoni kabisa kuona kwamba story za suala hili la miji 28 sasa linafikia ukingoni. Tumshukuru sana Mheshimiwa Rais ameweza kusimamia kwa karibu suala hili mpaka linaelekea ukingoni. Ahsante. (Makofi)