Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 2 Water and Irrigation Wizara ya Maji 20 2021-11-03

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itakamilisha Mradi wa Maji katika Vijiji vya Ikelu, Ibatu, Mtulingala, Nyamande, Usetule Mahongole Wilayani Makambako?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Deo Kasenyenda, Mbunge wa Jimbo la Makambako, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na utekelezaji wa miradi ya maji katika vijiji vya Ikelu, Ibatu, Mtulingala, Nyamande, Usetule na Mahongole. Utekelezaji wa mradi wa maji katika Kijiji cha Ikelu umefikia asilimia 98 na umeanza kutoa huduma ya maji kwa wananchi wa kijiji husika. Kazi zilizobaki ni ulazaji wa bomba umbali wa kilometa 29.8, ujenzi wa tanki la maji lenye ujazo wa lita 25,000 na ufungaji wa pampu unatarajiwa kukamilika ifikapo mwishoni mwa mwezi Desemba, 2021.

Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa mradi wa maji katika Kijiji cha Ibatu umefikia asilimia 56 ambapo kazi zilizobaki ni ukamilishaji wa ujenzi wa tanki la kuhifadhia maji lenye ujazo wa lita 100,000, ufungaji wa pampu ya kusukuma maji pamoja na uunganishaji wa umeme. Mradi huo umepangwa kukamilika mwezi Machi, 2022. Aidha, utekelezaji wa miradi katika Vijiji vya Mtulingala - Nyamande - Mbugani na Usetule – Mahongole kwa pamoja umefikia asilimia 67 na inatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Machi, 2022.

Mheshimiwa Spika, kukamilika kwa utekelezaji wa miradi hiyo kutaboresha huduma ya upatikanaji wa maji na kunufaisha wananchi wapatao 18,000 wa vijiji hivyo.