Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Simon Songe Lusengekile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa kipaumbele kwa Wilaya ya Busega kujengewa Mahakama ya Wilaya ili kuondoa usumbufu ambao wananchi wanaupata kwa kusafiri hadi Wilaya ya Bariadi kufuata huduma hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE: Mheshimiwa Spika, niishukuru sana Serikali kwa hatua za haraka ilizochukua. Ninavyozungumza sasa tayari msingi wameshaanza kuchimba. Pamoja na hayo, kwa kuwa kutoka Busega kwenda Bariadi ambako sasa kesi hizi zinaendeshwa za Kiwilaya ni kilometa takriban 70 na pale Makao Makuu ya Wilaya tuna jengo la Mahakama ya Mwanzo.

Je, Serikali sasa haioni haja ya kuturuhusu kutumia jengo lile angalau kwa hiki kipindi ambapo bado tunasubiri jengo letu kukamilika, kusikiliza kesi za kiwilaya ili kuondoa huu usumbufu wa wananchi kwenda Bariadi na kutumia gharama kubwa ambazo wakati mwingine wanashindwa kuzimudu? (Makofi)

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Simon Songe, Mbunge wa Busega kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli, pale kuna Mahakama ya Mwanzo, lakini vigezo vile vya kuitumia kama Mahakama ya Wilaya ndiyo kidogo vinakinzana, kwa hiyo waendelee kuvumilia ili tutakapokamilisha jengo lenye sifa, waweze kuanza kulitumia rasmi. Ahsante.

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa kipaumbele kwa Wilaya ya Busega kujengewa Mahakama ya Wilaya ili kuondoa usumbufu ambao wananchi wanaupata kwa kusafiri hadi Wilaya ya Bariadi kufuata huduma hiyo?

Supplementary Question 2

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Changamoto ambayo inawapata wananchi wa Busega inafanana kabisa na changamoto ambayo inawapata wananchi wa Jimbo la Momba.

Je, ni lini Serikali itaona kuna haja ya kutupa upendeleo ili tuweze kupata Mahakama yenye hadhi ya wilaya ili kuwapunguzia wananchi changamoto ya mwendo mrefu kufuata huduma za Mahakama kutoka Jimbo la Momba mpaka Mji wa Tunduma? Ahsante. (Makofi)

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Condester Sichalwe kutoka Jimbo la Momba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kimsingi katika Mpango Kazi wa kuendeleza ujenzi wa hizi Mahakama zetu za wilaya, 2022/ 2023 tunakwenda kuanza ujenzi wa Mahakama yake ya Momba ili kumpunguzia hiyo adha ambayo wananchi wanaikabili kwa sasa.