Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 5 Sitting 1 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 9 2021-11-02

Name

Simon Songe Lusengekile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatoa kipaumbele kwa Wilaya ya Busega kujengewa Mahakama ya Wilaya ili kuondoa usumbufu ambao wananchi wanaupata kwa kusafiri hadi Wilaya ya Bariadi kufuata huduma hiyo?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Simon Songe Lusengekile, Mbunge wa Busega, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ujenzi wa Mahakama ya Busega ni moja ya miradi itakayojengwa katika Mwaka wa Fedha 2021/2022. Mkandarasi wa ujenzi wa Mahakama hii amepatikana ambaye ni United Builders na kukabidhiwa eneo la ujenzi mwezi Oktoba. Kazi za ujenzi zimeanza na zinatarajiwa kukamilika ifikapo Aprili, 2022.

Mheshimiwa Spika, Mahakama ya Tanzania inaendelea kutekeleza programu ya maboresho ya majengo ya Mahakama zake na kukarabati majengo ya Mahakama katika ngazi mbalimbali za Mahakama hapa nchini ili kusogeza huduma karibu na wananchi na kuboresha mazingira ya kazi. Ahsante.