Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Regina Ndege Qwaray

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. REGINA N. QWARAY K.n.y. MHE. DANIEL B. SILLO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamaliza mgogoro wa mpaka kati ya Kiwanda cha Mbolea cha Minjingu na Vjiji vya Olacity na Minjingu?

Supplementary Question 1

MHE. REGINA N. QWARAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Je, Serikali imejipangaje kutatua mgogoro unaofanana na huo katika Vijiji vya Magara na mashamba ya wawekezaji kule Kiru?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; Serikali itakuja lini kutatua mgogoro katika vijiji vya Kata ya Kaiti ambavyo ni Vijiji vya Minjingu, Vilima Vitatu na Kakoi kati ya wafugaji na Jihubi? Ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Regina Ndege Qwaray, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu swali lake la kwanza na la pili ameainisha baadhi ya maeneo akisema Vijiji vya Magara na mashamba ya wawekezaji na hilo eneo lingine katika Mkoa wa Manyara. Katika maagizo ambayo sisi Serikali tumeyatoa ni kwamba tutaagiza Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na haya maeneo aliyoyataja, basi waende kutafutia ufumbuzi na watatuletea taarifa Ofisi ya Rais, TAMISEMI ili tujue hatua zaidi za kuchukua. Hata hivyo, tunaamini kwamba yapo ndani ya ofisi ya mkoa na wanaweza kuyamaliza na hii migogoro isiendelee.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Silinde, Naibu Waziri TAMISEMI, na kwa niaba ya Waziri, nataka niongeze kidogo majibu kwa Mheshimiwa Mbunge kwa kumpa taarifa kwamba viongozi wa Chama Cha Mapinduzi wa Mkoa wa Manyara wakiongozwa na Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Mkoa walikuja kuniona juzi kueleza hayo matatizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimewaahidi kwamba mwezi Oktoba tutakwenda kuitisha mkutano wa Viongozi wote wa Mkoa watuambie kwa pamoja matatizo yote yanayowasibu juu ya migogoro yao yote, halafu tupange ratiba ya kutekeleza kwa pamoja, pamoja na haya aliyoyasema. Hii ni nyongeza ya haya. Maagizo ya kwa Mkuu wa Mkoa tutayapeleka, lakini na mimi mwenyewe nitakwenda mwezi Oktoba. (Makofi)