Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 8 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 97 2021-09-09

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. REGINA N. QWARAY K.n.y. MHE. DANIEL B. SILLO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itamaliza mgogoro wa mpaka kati ya Kiwanda cha Mbolea cha Minjingu na Vjiji vya Olacity na Minjingu?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Daniel Baran Sillo, Mbunge wa Jimbo la Babati Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, mgogoro kati ya Kiwanda cha Mbolea cha Minjingu na Vijiji vya Olacity na Minjingu ulitokana na vijiji kutokutambua mipaka halisi kati ya vijiji hivyo na kiwanda, hivyo kusababisha wananchi kutoka katika vijiji hivyo kuingia na kufanya maendeleo katika eneo la kiwanda.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mwezi Januari, 2021 Serikali ilifanya uhakiki wa mpaka wa Kiwanda cha Minjingu na vijiji vinavyozunguka kiwanda hicho na kubaini kuwa kuna jumla ya kaya 83 ndani ya eneo la kiwanda ambapo kaya kutoka Vijiji vya Olacity na Minjingu ni miongoni mwa vijiji hivyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, miongoni mwa kaya hizo, kaya 40 za wahanga wa mafuriko ambazo ziliombewa na Kijiji cha Minjingu makazi ya muda ndani ya eneo la kiwanda, lakini baada ya muda wa makubaliano kuisha, kaya hizo zimegoma kuondoka katika eneo la kiwanda, hivyo kusababisha kuwepo kwa mgogoro huo.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaielekeza Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Manyara kukutana na pande zote mbili zinazohusika ili kuutafutia ufumbuzi mgogoro huo ifikapo Desemba, 2021.