Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya Hayati Dkt. John Pombe Magufuli ya ujenzi wa Barabara ya Bugene kupitia Pori la Kimisi hadi Benaco kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, ninalo swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba commitment ya Serikali, ni lini itajenga hizi kilometa 128.5 za barabara hii kupitia Pori la Kimisi hadi Benaco Ngara kwa kiwango cha lami? Kwa sababu nilishauliza mara nyingi sana ndani ya Bunge hili, najibiwa upembuzi yakinifu, upembuzi yakinifu, sasa naomba commitment ya Serikali.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. GODFREY
K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Oliver Daniel Semuguruka, Mbunge wa Viti Maalum, Kagera kwamba siyo tena tunaongelea upembuzi yakinifu ama usanifu wa kina. Naomba nimhakikishie kwamba tupo kwenye hatua za manunuzi. Mkandarasi wa barabara hii ameshapatikana na tupo kwenye majadiliano namna ya kuanza hii barabara.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nimtoe wasiwasi kwamba jinsi anavyofuatilia tutaanza na kilometa 60 kuanzia Bugene kuelekea Kasulo, yaani Benaco. Kwa hiyo, siyo tena habari ya kubabaisha, ni habari ya ukweli kwa sababu tayari tupo kwenye hatua za manunuzi. Kwa hiyo, awe na uhakika kwamba kazi anayofanya kufuatilia, sisi tunafanya na fedha hii tayari imeshatengwa kwa ajili ya kuanza ujenzi huo. Ahsante. (Makofi)

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya Hayati Dkt. John Pombe Magufuli ya ujenzi wa Barabara ya Bugene kupitia Pori la Kimisi hadi Benaco kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa barabara ya Iguguno – Sibiti yenye urefu wa kilometa 102 ina ahadi ya Mheshimiwa Hayati Dkt. John Pombe Magufuli Rais wa Awamu ya Tano: Je, ni lini Serikali itaanza kujenga barabara hii kwa kiwango cha lami ili kuharakisha shughuli za maendeleo kwa wananchi wa Jimbo la Iramba Mashariki na Mkoa wa Simiyu?

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. GODFREY
K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Aysharose Mattembe, Mbunge wa Viti Maalum, Singida, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara aliyoitaja ni ahadi ya viongozi wetu na pia ni barabara muhimu sana kwa uchumi wa Mkoa wa Singida, Simiyu, Mara na hata Manyara. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hii ni kati ya barabara ambazo zina barabara nyingi ambapo tayari kwenye bajeti ya mwaka uliopita tumepitisha kuanza kujenga hii barabara kwa sehemu. Ili tuanze kukamilisha hii barabara na katika hili daraja la Simiti, tayari tutakamilisha ujenzi kwa kiwango cha lami kwa barabara za maingilio. Kwa hiyo, nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Aysharose kwamba Serikali mwaka huu wa fedha kama tulivyoahidi kwenye bajeti na pia kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi tutaanza ujenzi kwa kiwango cha lami kwa sababu upembuzi yakinifu na usanifu wa kina tayari umeshafanyika.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. (Makofi)

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya Hayati Dkt. John Pombe Magufuli ya ujenzi wa Barabara ya Bugene kupitia Pori la Kimisi hadi Benaco kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. MAIMUNA S. MTANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nami naomba kumwuliza Mheshimiwa Naibu Waziri swali kuhusiana na barabara ya kutoka Amkeni – Kitangali hadi Mtama yenye kilometa 74.23 ambayo imeshajengwa kwa lami kwa kilometa 22.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa tunaomba commitment ya Serikali ni lini itatafuta fedha kutoka kwa wadau wengine wa maendeleo ili barabara kipande kilichobaki kiweze kukamilishwa kwa kiwango cha lami kwa sababu Serikali imekuwa ikitenga fedha kidogo, inajenga kilometa tatu tu kwa mwaka?

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kupata jibu. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. GODFREY
K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Maimuna Mtanda, Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba hii barabara aliyoitaja ya Amkeni kwenda Kitangali, tumekuwa tukitenga fedha kidogo kwa ajili ya ujenzi, lakini yote hii ni kutokana na uwezo wa bajeti. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inaendelea kutafuta vyanzo vingine vya fedha kwa ajili ya kujenga barabara, siyo hii tu bali ni barabara zote, kwamba kadri fedha inavyopatikana, basi Serikali itaongeza fedha. Ndiyo maana hata tukitangaza barabara pengine kilometa tatu, lakini fedha ikipatikana Serikali hatusiti kuongeza bajeti kwa ajili ya kuendeleza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba pamoja na barabara hii, kadri fedha itakavyopatikana, Serikali itazidi kuongeza kiasi cha fedha. Ahsante.