Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 7 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 89 2021-09-08

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya Hayati Dkt. John Pombe Magufuli ya ujenzi wa Barabara ya Bugene kupitia Pori la Kimisi hadi Benaco kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Oliver Daniel Semuguruka, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeanza kutekeleza ahadi ya Rais ya ujenzi wa barabara ya Bugene kupitia Pori la Kimisi hadi Benaco kwa kiwango cha lami ambapo upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara ya Bugene – Kasulo – Kumunazi yenye urefu wa kilometa 128.5 ulikamilika mwaka 2019. Taratibu za manunuzi ya Mkandarasi wa ujenzi wa sehemu ya Bugene – Burigi Chato National Park yenye urefu wa kilometa 60 zipo katika hatua ya mwisho kwa kutumia fedha za ndani. Katika mwaka wa fedha huu wa 2021/2022 shilingi bilioni tatu zimetengwa kwa ajili ya kazi hiyo.

Aidha, Serikali imewasilisha Benki ya Maendeleo ya Afrika maombi ya fedha za ujenzi kwa sehemu iliyobaki ya Burigi Chato National Park hadi Kumunazi yenye urefu wa kilometa 68.5. Ahsante.