Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Najma Murtaza Giga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NAJMA MURTAZA GIGA aliuliza: - Je, Serikali haioni umuhimu wa kuanzisha somo maalum la maadili kuanzia shule za msingi sambamba na somo la afya kwa mtoto ili kukabiliana na mabadiliko ya maumbile ya hisia za mwili pindi mtoto anapoanza kukua ikiwa ni njia ya kukabiliana na tatizo la watoto kuanza kushiriki mapenzi mapema?

Supplementary Question 1

MHE. NAJMA MURTAZA GIGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri sana ya Serikali, nitakuwa na maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza; pamoja na kutoa elimu hii katika shule zetu bado suala la mimba za utotoni ni changamoto katika jamii. Je, Serikali haioni umuhimu wa kufanya utafiti tunakosea wapi na wakati masomo yote tunatoa kwa watoto wetu? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; ni kuhusu Uraia. Tuna Somo la Uraia kuanzia elimu ya msingi hadi kidato cha sita, lakini suala la uzalendo limeondoka miongoni mwa wananchi wetu. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuweka mada maalum ya uzalendo kwenye Somo la Uraia?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA:
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Najma Murtaza Giga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimwondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inaendelea kufanya utafiti na kutilia mkazo juu ya masuala haya ya maadili. Kwa kuliona hilo katika miaka ya nyuma wanafunzi wetu wa shule za msingi walikuwa wanafanya mitihani katika masomo matano, lakini katika mwaka huu katika mitihani ambayo imeanza leo kwa kuona umuhimu wa somo hili la maadili tumeanza sasa kulifanyia mitihani ili kulijengea uwezo na kulitilia msisitizo zaidi. Kwa hiyo nimwondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge kwamba tunafanya utafiti na kwa umuhimu wa masomo haya imeonekana ni vyema vilevile nayo yakawa sehemu ya mitihani ya wanafunzi wetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hili, nitoe wito tu kwa ndugu wazazi na walezi; jukumu la malezi ya watoto ni la jamii nzima, siyo la shule wala Walimu peke yake. Hivi sasa imetokea tabia na mtindo kwamba majukumu sasa ya malezi ya watoto wetu yamekuwa ya shule peke yake. Kwa hiyo tutoe wito kwamba, majukumu haya ni ya kwetu kuhakikisha kwamba maadili ya watoto wetu pamoja na mienendo ya taaluma zao tunafuatilia kwa karibu.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika eneo la pili, kwamba Serikali sasa tuna mpango gani? Nimtoe wasiwasi vilevile Mheshimiwa Mbunge na Waheshimiwa Wabunge wote, mchakato tunaoendelea nao sasa wa kuboresha mitaala yetu, mambo haya yote tutayatilia mkazo. Waheshimiwa Wabunge mna nafasi nzuri ya kutoa mawazo yenu ili kuweza kuangalia namna gani tunaweza tukatengeneza maadili, lakini tukaweka taaluma vizuri kwa vijana wetu kuhakikisha kwamba tunahitaji kizazi gani chenye maadili gani cha huko mbele tunakokwenda.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.

Name

Philipo Augustino Mulugo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songwe

Primary Question

MHE. NAJMA MURTAZA GIGA aliuliza: - Je, Serikali haioni umuhimu wa kuanzisha somo maalum la maadili kuanzia shule za msingi sambamba na somo la afya kwa mtoto ili kukabiliana na mabadiliko ya maumbile ya hisia za mwili pindi mtoto anapoanza kukua ikiwa ni njia ya kukabiliana na tatizo la watoto kuanza kushiriki mapenzi mapema?

Supplementary Question 2

MHE. PHILLIPO A. MULUGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Swali langu la nyongeza kwa Wizara ya Elimu, pamoja na Wizara ya Afya ni kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, miaka ya nyuma kidogo huko shuleni kulikuwa na utaratibu wa kuwapima mimba wanafunzi kuanzia darasa la sita, la saba na hata sekondari, lakini miaka ya hivi karibuni nimekosa kumbukumbu ni kama suala hilo halipo, kwa sababu na mimi ni mdau wa elimu, labda kama wanapima kwenye shule za Serikali. Je, kwa nini Serikali haioni umuhimu wa kuanza kupima mimba angalau mara mbili kwa mwaka kuanzia darasa la sita, la saba na upande wa sekondari ili kuwaweka wanafunzi wa kike hata wa kiume kuwe na tension fulani kwamba kuna kupima mimba mara mbili kwa mwaka na kuacha mimba za utotoni?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA:
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Mulugo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, utaratibu huu kimsingi upo pindi watoto wetu wanapotoka likizo tunafanya utaratibu huo. Sasa nimtoe wasiwasi tu Mheshimiwa Mbunge, labda tuweze kuendelea kuutilia tu msisitizo na mkazo ingawa hatuufanyi in public, unafanyika kule shuleni na kinakuwa kitu ambacho ni cha kishule zaidi kuliko kutangaza, lakini kimsingi ni utaratibu ambao upo unatumika kwenye shule zetu za Serikali, vijana wetu wanapotoka likizo huwa utaratibu huo unakuwepo. Hata hivyo, tuchukue vilevile wazo lake, tuendelee kuliimarisha na kuliboresha tuweze kuangalia namna gani ya kufanya. Ahsante sana.