Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 7 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 88 2021-09-08

Name

Najma Murtaza Giga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NAJMA MURTAZA GIGA aliuliza: -

Je, Serikali haioni umuhimu wa kuanzisha somo maalum la maadili kuanzia shule za msingi sambamba na somo la afya kwa mtoto ili kukabiliana na mabadiliko ya maumbile ya hisia za mwili pindi mtoto anapoanza kukua ikiwa ni njia ya kukabiliana na tatizo la watoto kuanza kushiriki mapenzi mapema?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Najma Murtaza Giga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara inatambua umuhimu wa kufundisha maadili kwa mtoto ili kukabiliana na mabadiliko ya maumbile ya hisia za mwili kama njia ya kukabiliana na tatizo la watoto kuanza kushiriki mapenzi mapema.

Mheshimiwa Naibu Spika, mitaala ya elimu inayotumika kwa sasa imetilia msisitizo kuhusu masuala ya maadili katika ngazi zote za elimu. Katika ngazi ya elimu ya msingi kuna Somo la Uraia na Maadili ambalo ni somo la lazima kwa wanafunzi wote kuanzia darasa la tatu.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile, suala la mabadiliko ya maumbile ya mtoto hufundishwa katika Somo la Sayansi na Teknolojia, Stadi za Kazi, na Uraia na Maadili. Katika ngazi ya sekondari masuala ya maadili hufundishwa katika Somo la Civics Kidato cha kwanza mpaka cha nne na katika Somo la General Studies Kidato cha tano na cha sita. Masomo haya ni ya lazima kwa wanafunzi wote wa sekondari. Aidha, masuala ya afya hufundishwa katika Somo la Biologia ambalo pia ni somo la lazima kwa wanafunzi wote wa Kidato cha kwanza mpaka cha nne.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea na zoezi la kuboresha mitaala kwa ngazi za elimu ya awali, msingi na sekondari. Zoezi hilo linahusisha kupokea maoni ya wadau ambayo yatazingatiwa katika maboresho ili kuhakikisha mitaala yetu inakidhi mahitaji na inawajengea wanafunzi maadili ya Kitanzania. Ahsante sana.