Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza: - Je, ni lini ahadi ya Mheshimiwa Rais ya Mwaka 2015 ya ujenzi wa Kivuko cha Mto Kalambo itatekelezwa?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Naomba pia nishukuru kwa majibu ya Serikali.

Mheshimiwa Naibu Spika, majibu ya Serikali yanakiri kwamba upembuzi yakinifu ulifanyika mwaka 2018 ambapo aliyekuwa Makamu wa Rais ambaye ndiye Rais wa sasa naye alikuja kutoa ahadi. Swali; natakiwa kuikumbusha mara ngapi Serikali ili ujenzi uanze?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Ni ukweli usiopingika kwamba pale ambapo maeneo yetu na mikoa yetu inapopata fursa ya kutembelewa na viongozi wa Kitaifa kuna mambo ambayo tunanufaika ikiwa ni pamoja na ahadi za viongozi hao wa kitaifa. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba hawa viongozi wa kitaifa wanapangiwa ziara ili kutembelea mikoa yote ili na sisi tuweze kufaidika katika ahadi ambazo wanatoa viongozi hao?

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kujibu maswali madogo ya nyongeza ya Mheshimiwa Josephat Sinkamba Kandege, Mbunge wa Jimbo la Kalambo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa tunakubaliana na mawazo yake Mheshimiwa Mbunge. Ni kweli Serikali imeshafanya kazi ya awali ya kuandaa detail design na imeshakamilika; na kama ambavyo nimemjibu katika swali langu la msingi hapa, nilimwambia kwamba sasa hivi kazi ambayo tunaifanya Serikali ni kutafuta fedha tu ili daraja hilo lianze kujengwa, hicho kivuko ambacho tumekitaja hapo. Kwa hiyo nimwambie tu kwamba hahitaji kuikumbusha Serikali mara kwa mara kwa sababu Serikali ya Awamu ya Sita ni Serikali makini inakumbuka kila ahadi ambayo tumeitoa. Kwa hiyo na kwenye hili nimwondoe shaka kabisa kwamba fedha itakapopatikana tutakamilisha ujenzi huo, na ninaamini ndani ya kipindi hiki cha miaka 5 ya Mheshimiwa Rais wetu tutalitekeleza hilo.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili linalohusu ziara za viongozi, ninaamini hapa anazungumzia Mawaziri, Naibu Mawaziri, na hususan Ofisi yetu ya Rais TAMISEMI. Nimuahidi tu kwamba nitafika katika eneo lake na tutafanya ziara ya pamoja kwenda kujionea shughuli za kimaendeleo zinazofanyika eneo lile ahsante sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.