Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 7 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 81 2021-09-08

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Primary Question

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza: -

Je, ni lini ahadi ya Mheshimiwa Rais ya Mwaka 2015 ya ujenzi wa Kivuko cha Mto Kalambo itatekelezwa?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Josephat Sinkamba Kandege Mbunge wa Jimbo la Kalambo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, utekelezaji wa ahadi ya Mheshimiwa Rais ya mwaka 2015 na vilevile ahadi ya Mheshimiwa Makamu wa Rais ya mwaka 2020 ambaye kwa sasa ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan umeanza, ambapo upembuzi yakinifu (Detailed Design) wa kivuko hicho umekamilika mwaka 2018, ambao ulifanywa na Mhandisi Mshauri Advanced Engineering Solutions Limited ya Tanzania kwa kushirikiana na Teknicon Limited ya Tanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa Kivuko hicho chenye urefu wa mita 80 unategemea kugharimu Shilingi Bilioni Nne milioni mia sita themanini na tisa mia saba themanini na tatu elfu mia saba kumi na mbili na senti hamsini.

Mheshimiwa Naibu Spika, hatua iliyofikia sasa ni kwa Serikali kuendelelea kutafuta fedha za ujenzi wa kivuko hicho, pindi fedha zitakapopatikana ujenzi utaanza mara moja.