Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO K.n.y. MHE. NORAH W. MZERU aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka mashine za incubator za kutosha nchini ili kuzuia vifo vya watoto?

Supplementary Question 1

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa hii nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Mheshimiwa Waziri amekiri kwamba kuna uchache ama upungufu mkubwa wa hizi mashine za incubator; na anasema kwamba hakuna utafiti wa kisayansi ambao unaonesha kwamba zinaweza kusaidia maisha ya Watoto; je, yuko tayari kuleta utafiti wa kisayansi kuelezea mahusiano ya vifo vya watoto njiti kwa kukosa huduma hasa kwa kutokuwepo kwa hizi incubators?

Mheshimiwa Spika, swali la pili: Kama wametambua kwamba Kangaroo Mother Care imekuwa ni njia mujarabu katika kuokoa maisha ya watoto, ni juhudi gani za Serikali zimechukuliwa kuhakikisha elimu hii inafika vijijini ili kuokoa maisha ya watoto? (Makofi)

Name

Dr. Dorothy Onesphoro Gwajima

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Ahsante sana Mheshimiwa Londo kwa maswali yako mawili mazuri kabisa. Napenda kujibu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, scientific data au scientific evidence kuhusu eneo hili zipo na sayansi huwa inaendelea kufuatilia mambo mbalimbali kadri muda unavyokwenda na ku-adapt marekebisho ili kuboresha. Hivyo, kwa ridhaa yako, kama tutapata fursa tunaweza tukawasilisha kupitia Kamati ya Huduma za Jamii baadaye ikafika Bungeni, hizi tafiti mbalimbali zilizofikia, tukafanya adjustment siyo tu Tanzania, dunia nzima, kwenye eneo hili.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa elimu kufika vijijini, tayari tulishatoa mwongozo wa maboresho eneo hili, upo; na kupitia Waganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya tutahakikisha tunasogeza elimu hii kwenye jamii ili waweze kuona umuhimu wa kukaa na mtoto kifuani kwao, hasa anapokuwa amezaliwa na uzito pungufu sana tuendelee kuokoa maisha. Hii imeonesha kwenye data zetu za mwaka 2018 mpaka 2020 vifo vimeendelea kupungua kutoka 11,524 mpaka 8,190. Ni katika mikakati hii ambayo tumeichukua ya kuhakikisha kwamba tunaokoa maisha ya watoto.

Name

Mwanaisha Ng'anzi Ulenge

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO K.n.y. MHE. NORAH W. MZERU aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka mashine za incubator za kutosha nchini ili kuzuia vifo vya watoto?

Supplementary Question 2

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa nafasi ya swali la nyongeza; na nitauliza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mashine ya kupima kiwango cha usikivu kwa watoto mara wanapozaliwa (auditory brainstem response test) ipo Muhimbili peke yake hapa nchini. Hospitali zote za rufaa nchini hazina kifaa hiki, sasa ili kuipunguzia Serikali mzigo wa kuhudumia wanafunzi wenye ububu na uziwi na kuendesha kwa gharama kubwa shule hizo: Je, Serikali haioni haja ya kuhakikisha kwamba mashine hizo zinapatikana na inakuwa ni lazima kwa kila mtoto anayezaliwa kupimwa kiwango chake cha usikivu?

Name

Dr. Dorothy Onesphoro Gwajima

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa swali zuri la Mheshimiwa Engineer Mwanaisha, Mbunge, kuhusu masuala ya kuwapima watoto kiwango cha usikivu pale wanapozaliwa, kwamba ni gharama sana kwa sababu ni hadi uende Muhimbili. Nakubaliana kabisa na ninampongeza kwa kuliona hili.

Mheshimiwa Spika, niweze tu kusema haja ipo na ndiyo maana Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan imeendelea kuboresha miundombinu ya hospitali za kibingwa, hasa za kanda ili kusogeza siyo tu vifaa, pamoja na hawa wataalam wanaotakiwa kupima. Tuna hospitali yetu ya Mtwara imeshafikia asilimia 95, tuna ya Chato inakamilika, pia tuna Meta Mbeya inakamilika.

Mheshimiwa Spika, ni pendekezo la msingi na ni hoja ya msingi sana. Katika bajeti inayokuja tutaanza kuona kadri tunavyozindua, hata hawa wataalam wanaoshughulika na masuala ya usikivu, tuendelee kuwapa training tuwasogeze kwenye hospitali hizo. Ahsante.