Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya Ujenzi wa Barabara za Kwasadala – Jiweni, Mashua - Shirinjoro –Mijongweni, Kalali – Nronga, Arusha Road – Mlimashabaha –Sanya Stastesheni pamoja na Kwasadala – Uswaa?

Supplementary Question 1

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, kwa kuwa kipande cha barabara ya Mashua – Jiweni ni kipande muhimu sana kwa sababu kinahudumia Kata tatu; Kata za Masama Kusini, Romu na Masama Magharibi lakini Vijiji vikubwa vya Lukani, Kiu, Lwasaa na Jiweni. Barabara hii kwa sasa haipitiki, je, Serikali haioni ipo haja ya kupeleka fedha za dharura ili barabara hii ambayo inatuletea mazao huku Dodoma, iweze kupitika?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa tangia tumepata Uhuru, Jimbo la Hai hatujawahi kupata taa za barabarani, ni lini sasa Serikali itatuletea taa za barabarani kwenye Mji mkubwa unaokua wa Boma Ng’ombe, Maili Sita na Njia Panda ya kwenda Machame? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Saashisha Elinikyo Mafuwe, Mbunge wa Jimbo la Hai, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge ameuliza hapa kwamba barabara ya Mashua mpaka Jiweni ambayo inahudumia Kata kubwa tatu haipitiki na ameomba fedha za dharura. Nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge tumelipokea ombi lake na tutakachokifanya sasa hivi tutatuma wataalam wakafanye tathmini na baada ya hapo tutatafuta fedha ili barabara hiyo iweze kutengenezwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, ni lini sasa Serikali itapeleka taa za barabarani katika Miji Mikubwa ya Boma Ng’ombe, Njia Sita pamoja na Kata nyingine ambazo ameanisha hapa. Niseme tu najua jitihada kubwa za Mheshimiwa Mbunge kwa Jimbo la Hai na najua ana dhamira ya kweli ya kuwasaidia wananchi wake, kwa sababu ameleta ombi hili niseme na lenyewe tunalipokea kwa ajili ya kulifanyia kazi. Naamini kabisa kwa ufuatiliaji wake mzuri na fedha ikipatikana basi taa zitaletwa na Serikali kwa wakati kulingana na bajeti itakavyopatikana. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya Ujenzi wa Barabara za Kwasadala – Jiweni, Mashua - Shirinjoro –Mijongweni, Kalali – Nronga, Arusha Road – Mlimashabaha –Sanya Stastesheni pamoja na Kwasadala – Uswaa?

Supplementary Question 2

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kuniona. Nadhani mtakubaliana nami kwamba hizi barabara zinajengwa ili kuwapa watu urahisi wa maisha na kuwawezesha.

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya kutoka Kalali – Nronga ni barabara ambayo ina kona nyingi, ni ndefu na ina milima, ni chini tu ya Mlima Kilimanjaro. Huko Nronga ndiyo kwenye kile kiwanda kikubwa cha maziwa ya mgando ambayo pia yananywewa hapa Dodoma. Swali langu kwa Wizara, ni lini sasa barabara hiyo itaanza kutengenezwa kidogokidogo kwa lami ili wamama wale waweze kuteremsha maziwa yao mpaka mjini na kufika huku Dodoma kwa ajili ya afya za watu? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Shally Raymond, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli anachokieleza Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara ya Kalali – Nronga ambayo inapita pembezoni mwa Mlima Kilimanjaro kule chini imeharibika na tunahitaji fedha ya kutosha kuendelea kuijenga na ombi la Mheshimiwa Mbunge ni kwamba wanahitaji sasa ianze kujengwa polepole kwa kiwango cha lami. Niseme tu kwamba kulingana na bajeti yetu kadri itakavyoongezeka, tutalipokea na tutaliweka katika mipango yetu ya baadaye kuhakikisha barabara hii inatengenezeka ili iweze kutoa huduma kwa urahisi kwa wananchi wa eneo husika. Ahsante sana.