Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 62 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 520 2021-06-30

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya Ujenzi wa Barabara za Kwasadala – Jiweni, Mashua - Shirinjoro –Mijongweni, Kalali – Nronga, Arusha Road – Mlimashabaha –Sanya Stastesheni pamoja na Kwasadala – Uswaa?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Saashisha Elinikyo Mafuwe, Mbunge wa Jimbo la Hai, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara za Kwasadala –Jiweni – Mshua, barabara ya Shirinjoro – Mijengweni, barabara ya Kalali – Nronga, Arusha Road - Mlima Shabaha – Sanya Stastesheni pamoja na Kwasadala – Uswa zimesajiliwa kwa majina ya Kwasadala - Mshua yenye urefu wa kilomita 35.06, barabara ya Shirinjoro - Mijongweni yenye urefu wa kilomita 12.71, barabara ya Kalali - Nronga yenye urefu wa kilomita 6.04, barabara ya Somali - Tindigani yenye urefu wa kilomita 12.00 na Barabara ya Kwasadala - Uswaa yenye urefu wa kilomita 9.87.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2019/2020, Serikali kupitia TARURA, Halmashauri ya Wilaya ya Hai imezifanyia matengenezo barabara za Kwasadala - Mashua kilomita 14, Shirinjoro - Mijongweni kilomita 5, Kalali -Nronga kilomita 5 na barabara ya Kwasadala - Uswaa kilomita 5 kwa gharama ya shilingi milioni 157.5. Katika mwaka wa fedha 2020/2021, Serikali imetenga shilingi milioni 189.35 kwa ajili ya matengenezo ya barabara za Kwasadala - Mshua kilomita 17, Shirinjoro - Mijongweni kilomita 4, Kalali-Nronga kilomita 5 na barabara ya Kwasadala - Uswaa kilomita 9. Matengenezo ya barabara hizo yanaendelea na yanatarajiwa kukamilika ifikapo Agosti 2021.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022 barabara hizo zimetengewa shilingi milioni 123 kwa ajili ya matengenezo ya vipande vyenye jumla ya urefu wa kilomita 30.