Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya ujenzi wa madarasa ya Kidato cha Tano na Sita katika Shule ya Sekondari Bugando iliyopo Tarafa ya Bugando na Shule ya Sekondari ya Rubanga iliyopo Tarafa ya Isulwabutundwe?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Kwanza, niishukuru sana Serikali kwa kutusaidia pesa na kuweza kumalizia ujenzi wa madarasa ya Form Five na Six pale Nzela.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la kwanza, majibu ya Serikali kuhusiana na Shule ya Sekondari Lubanga hayajajitosheleza vizuri kwa kuwa tumekuwa tukisuasua, hata hayo madarasa mawili yamejengwa na Mbunge pamoja na nguvu za wananchi. Kwa sababu maombi nimeshaleta zaidi ya mara tano, ni lini Serikali mtatupatia pesa kwa ajili ya kujenga madarasa na mabweni kwa ajili ya Form Five na Six pale Lubanga? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, ili Mheshimiwa Naibu Waziri aone nachokiomba kina umuhimu, naomba commitment yake baada ya Bunge twende wote akaone ule umbali wa kutoka Lubanga kwenda kwenye hiyo shule ya Form Five na Six ambayo itafunguliwa mwezi waliopanga, ni kilometa 105, ni lini Mheshimiwa Naibu Waziri yupo tayari?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Joseph Kasheku Musukuma, Mbunge wa Jimbo la Geita, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza ametaka tu commitment ya Serikali kwamba ni lini sasa Shule ya Lubanga itapelekewa fedha ili yale madarasa mengine yakamilike na shule hii tuweze kuifungua kwa wakati. Nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge tumelipokea suala hili, tutatafuta fedha na tutaziweka katika miradi ambayo inafuatia ili kuhakikisha katika mwaka wa fedha unaokuja shule hii iwe imekamilika.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili alikuwa ananiomba tuweze kuongozana mara baada ya Bunge, nimpe taarifa kwamba nitakuwa na ziara katika Mkoa mzima wa Geita. Kwa hiyo, niseme tu kabisa kwamba nitakwenda pamoja naye mpaka katika eneo hili analolisema kujionea kwa pamoja. Ahsante sana.

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya ujenzi wa madarasa ya Kidato cha Tano na Sita katika Shule ya Sekondari Bugando iliyopo Tarafa ya Bugando na Shule ya Sekondari ya Rubanga iliyopo Tarafa ya Isulwabutundwe?

Supplementary Question 2

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuweza kuuliza swali dogo la nyongeza.

Kwa huwa Shule ya Sekondari Msalala tumeweza kujenga madarasa na miundombinu yote kwa ajili ya Kidato cha Tano na cha Sita na pia Kata ya Nyangh’wale tumeweza kukamilisha ujenzi huo.

Je, ni lini sasa Serikali itatoa kibali ili tuweze kufungua shule hizo kwa Kata za Nyang’wale na Msalala? Tumeshakamilisha miundombinu, ni lini Serikali itatoa kibali ili tuweze kufungua shule hizo?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Hussein Amar, Mbunge wa Nyang’wale, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, amesema katika eneo lao wameshamaliza ujenzi wa shule za sekondari katika Kata za Nyang’wale pamoja na Msalala na anachotaka kujua tu ni lini Serikali itatoa kibali. Kwa sababu ameshalizungumza hapa nitaagiza wataalam wangu waende wakafanye tathmini pale wajihakikishie kama miuondombinu yote imeshakamilika. Wakishajiridhisha na hilo maana yake tutatoa kibali mara moja na shule hiyo itafunguliwa. Ahsante sana. (Makofi)