Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 62 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 519 2021-06-30

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya ujenzi wa madarasa ya Kidato cha Tano na Sita katika Shule ya Sekondari Bugando iliyopo Tarafa ya Bugando na Shule ya Sekondari ya Rubanga iliyopo Tarafa ya Isulwabutundwe?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Kasheku Musukuma, Mbunge wa Jimbo la Geita, kama ifuatavyo: -

Mheshimwa Naibu Spika, Serikali kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Geita pamoja na wadau wa elimu imekamilisha ujenzi wa miundombinu ya Kidato cha Tano na Sita katika Shule ya Sekondari Bugando iliyopo katika Kata ya Nzera, Tarafa ya Bugando katika Jimbo la Geita. Shule hii imepata kibali cha kuanzisha Kidato cha Tano na Sita mwaka 2021 kwa michepuo ya PCM na PCB na imepangiwa wanafunzi wa kiume 124 wataoanza kuripoti mnamo tarehe 03 Julai, 2021.

Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Geita inaendelea na upanuzi wa Shule ya Sekondari Lubanga iliyopo katika Kata ya Isulwabutundwe, Tarafa ya Bugando ili iweze kuwa na Kidato cha Tano na Sita. Ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa upo katika hatua ya ukamilishaji na ujenzi wa matundu 12 ya vyoo unaendelea. Halmashauri kwa kushirikiana na wadau wa elimu inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa bweni.

Aidha, Halmashauri ya Wilaya ya Geita imekamilisha ujenzi wa madarasa 4 na ununuzi wa viti 160 na meza 160 katika Shule ya Sekondari Kakubilo na inaendelea na ujenzi wa bweni na bwalo la chakula.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kuboresha miundombinu ya Shule za Sekondari katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita na itazipatia kibali cha kupokea wanafunzi wa Kidato cha Tano na Sita mara baada ya kukamilisha ujenzi wa miundombinu muhimu.