Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Primary Question

MHE. DKT. STEVEN L. KIRUSWA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamalizia ujenzi wa kipande cha barabara ya lami kilichoanzia Sanya Juu kuelekea Kamwanga ambayo kwa sasa imeishia Kijiji cha Elerai wakati zimebaki takribani kilometa 44 kuunganisha na kipande kingine cha lami kilichotoka Tarakea na kuishia Kijiji cha Kamwanga?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. STEVEN L. KIRUSWA Mheshimiwa Naibu Spika, nakuskuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswli madogo mawili ya nyongeza.

Kwa kuwa barabara hii itakapokamilika itakuwa imekamilisha mzunguko wa Mlima Kilimanjaro kwa barabara ya lami, na hivyo itaongeza na kuchochea kasi ya ukuaji wa utalii wa Mlima Kilimanjaro na hifadhi ya Mlima Kilimanjaro vilevile. Kuna barabara nyengine ambayo ilipendekezwa kwenye ilani tangu mwaka 2015, inayotoka Longido kuja kuungana na hii ya lami katika eneo la Sanya Juu, na barabara hii pia itapita ndani ya Hifadhi ya Jamii ya Indumet.

Je, Serikali imeweka mpango gani wa kuhakikisha kwamba barabara hii ya kuunganisha hiyo Wilaya ya Longido na Mkoa wa Kilimanjaro na maeneo ya hifadhi na uzalishaji wa zao ya West Kilimanjaro inakwenda kujengwa?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa kuna barabara pia muhimu ya TANROADS inayotoka Longido mpaka Oldonyolengai mlima mwingine wa kitalii na maarufu duniani, pale ambapo itaungana na ile inayotoka Loliondo kuja mpaka Mto wa Mbu.

Je, Serikali itaanza lini kama ilivyo ahidiwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya 2020/2025 kufanya usanifu wa barabara ya lami kwa ajili ya barabara hiyo muhimu kwa biashara ya utalii?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, ninaomba kujibu swali moja la nyongeza ya Mheshimiwa Kiruswa, muhimu sana kama ifutavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge na Waheshimiwa Wabunge kwamba wote kwamba ahadi zote ambazo zipo kwenye Ilani ya Uchaguzi za Chama cha Mapinduzi na zile ambazo zinazotolewa na viongozi wakuu wa Serikali zitatekelezwa kama zilivyopangwa, hiyo ni kwa awamu kutokana na upatikanaji wa fedha.

Mheshimiwa naibu Spika, barabara mbili ambazo umezitaja zote ni muhimu sana, na unapojenga barabara hizi, hii Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi unajua ni Wizara wezeshi, ukijenga barabara pale Mlima Kilimanjaro, utaongeza idadi ya watalii na mapato yataongezeka na utekelezaji wa Ilani utatekelezwa vizuri zaidi.

Kwa hiyo Mheshimiwa Mbunge nikwambie kwamba barabara ya Longido-Sanya Juu itaanza kujengwa kadri tukipata fedha pia Longido Oldonyolengai ambayo umeitaja nayo ni muhimu sana na tutaifanyia kazi, lakini nikupongeze kwa kazi unayoifanya ya kuwasemea wananchi wako wa Jimbo lako, ahsante sana.

Name

Nicodemas Henry Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. DKT. STEVEN L. KIRUSWA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itamalizia ujenzi wa kipande cha barabara ya lami kilichoanzia Sanya Juu kuelekea Kamwanga ambayo kwa sasa imeishia Kijiji cha Elerai wakati zimebaki takribani kilometa 44 kuunganisha na kipande kingine cha lami kilichotoka Tarakea na kuishia Kijiji cha Kamwanga?

Supplementary Question 2

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, suala liliopo Longido hata Mbogwe lipo; na ni mpango wa Serikali kila Halmashauri kuunganisha barabara za lami kwenda Makao Makuu ya Mkoa.

Je, Wizara inampango gani kulingana na Jimbo langu la Mbogwe sina barabara inayounganishwa Wilaya kwa Mkoa? (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Maganga, Mbunge wa Mbogwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza Mheshimiwa Mbunge ni kweli kwamba tumekuwa tukizungumza mara kwa mara kufatilia ujenzi katika jimbo lake na tumeshawaelekeza Meneja wa TANROADS Mkoa ili waangalie mipango iliyoko ndani ya mkoa wao, lakini pia tuangalie na hii ya Wizara. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mpango uliopo wa Serikali ni kuunganisha Mkoa kwa Mkoa, Wilaya na Mkoa na Wilaya kwa Wilaya. Kwa hiyo hoja yako tumeipokea Mheshimiwa Mbunge tutaifanyia kazi kadri ambavyo Serikali itapata fedha. Ahsante.